Wednesday 3 December 2014

MWAMUZI TANZANIA AFUZU KUCHEZESHA AFCON YA VIJANA, SASA AWANIA YA WAKUBWA

 

Mwamuzi kutoka Tanzania, Samwel Mpenzu, amefuzu kuchezesha michuano mikubwa itakayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf) ikiiwemo ya Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 20 (Afcon U-20).

Mpenzu, ambaye ni mwamuzi mwenye beji ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), amefuzu baada ya kupita kwenye mchujo wa kupata nafasi hiyo ambao ulifanyika Cairo, Misri wiki iliyopita pamoja na waamuzi wengine kutoka nchi mbalimbali barani Afrika.
Mwamuzi huyo alisema kuwa baada ya kupita kwenye hatua hiyo, kwa sasa anachoangalia ni kupita kwenye hatua inayofuata ‘Elite A’ ambayo itamfanya aweze kuchezesha michuano ya wakubwa ya Afcon pamoja na Kombe la Dunia.

Alisema kuwa lengo lake kubwa ni kuchezesha Kombe la Dunia, kwani hakuna Mtanzania aliyefika huko.

0 comments: