Monday 19 May 2014

REAL MADRID WATAKA KUVUNJA TENA REKODI YA USAJILI DUNIANI KWA KUTOA PAUNI MILIONI 100 KUMNUNUA SUAREZ

MAGALACTICO, Real Madrid wanataka kutumia mbinu zao maarufu za kutangaza ofa nene, katika kuhakikisha inamnasa mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez na imesema iko tayari kutoa Pauni Milioni 100 ili kumpata.
Madrid, ambayo imekosa taji la La Liga na inakabiliwa na mtihani mwingine wa kumenyana na mabingwa weepy wa Hispania, Atletico Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wanataka kutumia mbinu zap ki-Galactico kwa kuanza kuvujisha habari zisizo rasmi juu ya mpoango huo.
Na magazeti ya kila siku ya michezo Hispania ndiyo yanaonekana kuwa silaha yao kuu. Lakini inafahamika Madrid inakabiliwa na mtihani mzito kwa sababu Liverpool haiko tayari kumuuza Suarez na wakati huo huo, wapinzani wao, Barcelona wanamtaka pia.
Atahamia Hispania? Luis Suarez anaweza kununuliwa kwa Pauni Milioni 100 na timu ya timu zinazomuwania, baina ya Barcelona na Real Madrid 

Kiwango cha of a ambayo Real inatake kutoa kwa ajili ya Suarez itakuwa rekodi mpya ya dunia na itakuwa vigumu kwa Liverpool kukataa dau hilo.
Licha ya panda zone kukanusha kwa maana ya mchezaji na klabu yake, lakini inaaminika kuna kiwango cha dau ambacho kikifikiwa Suarez anaweza kuuzwa kama atataka kuondoka. 
Hilo linatarajiwa kuwa sakata kubwa wakati wa uhamisho wa dirisha kubwa baada ya Fainali za Kombe ka Dunia.

0 comments: