Tuesday 5 August 2014

watu wawili wauawa kutokana na wivu wa kimapenzi wilayani Chunya.




Na Samwel Ndoni Mbeya,
WAKATI takwimu za jeshi la polisi mkoani Mbeya zikionesha matukio ya mauaji katika kipindi cha mwezi January mpaka juni mwaka huu, yalikuwa ni 135, huenda idadi hiyo ikaongezeka katika kipindi kijacho kama hiki kutokana na kuongezeka kwa visa hivyo mkoani hapa.

Hali hiyo inatokana na vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi kuzidi kushika kasi licha ya serikali na mashirika mbalimbali kukemea vitendo hivyo, kufuatia  watu  wawili kuuawa kutokana na wivu wa kimapenzi wilayani Chunya.

Tukio hilo limetokea katika kitongoji na kijiji cha Magamba wilayani humo ambapo mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Neema Mbuzi mkazi wa kitongoji hicho aliuawa na mume wake kwa kukatwa mapanga baada ya kumkuta  akiwa na mwanaume mwingine asiyefahamika wakiwa nyumbani kwake wakivunja amri ya sita.

Imeelezwa kijijini hapo kuwa mume wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Msafiri Shitindi alimfumania mkewe majira ya saa sita usiku ambapo hata hivyo mwanaume aliyeshikwa ugoni alikimbia.
Aidha baada ya Mgoni huyo kukimbia mtuhumiwa alimkamata mkewe na kuanza kumshambulia kwa kumtata mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababishia kifo chake.

Hata hivyo siku mbili baadae ndugu wa marehemu Neema aliyefahamika kwa jina la Mlawa alimuua mtuhumiwa kwa kosa la kumuua ndugu yake.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa niaba ya mwenyekiti wa kitongoji hicho mjumbe wa serikali ya Kitongoji cha Magamba Fikiri John  amesema kuwa mtuhumiwa Mlawa anashikiliwa na polisi kituo cha Mkwajuni kwa mahojiano zaidi.

0 comments: