Sunday 3 August 2014

MAN UNITED YAWAFUMUA REAL MADRID 3-1 KOMBE LA KIMATAIFA MAREKANI


MANCHESTER United imewafunga mabingwa wa Ulaya, Real Madrid mabao 3-1 katika Kombe la Kimataifa Uwanja wa Michigan mjini Ann Arbor, Detroit nchini Marekani. 
Shujaa wa United alikuwa ni winga Ashley Young aliyefunga mabao mawili- huku bao pekee la Real likifungwa Gareth Bale.
Young alifunga bao la kwanza kwa kikosi cha Louis van Gaal dakika ya 20, kabla ya Madrid kusawazisha kwa penalti kupitia kwa Bale dakikan ya 27.
Lakini Young tena akamuinua kitini kocha Van Gaal dakika ya 37 akiunganisha vizuri krosi kumtungua kipa Iker Casillas. Nyota wa zamani wa United, Cristiano Ranaldo ambaye kabla ya mcheo huo alisema hajawahi kukataa kurudi timu hiyo, aliingia dakika ya 74, lakini akashindwa kuisaidia timu yake. 
Umati wa mashabiki 109,00 ndani ya Michigan mjini Ann ArborBurst of pace: Gareth Bale draws a foul from Michael Keane inside the penalty area
Gareth Bale akimtoka Michael Keane Dictating play: Rooney put in a good performance for Van Gaal's side as they upset Madrid in Detroit
Rooney aling'ara jana mjini Detroit Friendly: Danny Welbeck and Pepe challenge for a cross as United have the best of the early exchanges
Danny Welbeck akipambana na beki 'mtata' PepeStar turn: The Portugal captain did not push himself too hard as he continues his preparations for the season
Ronaldo alishindwa kuiepusha na kipigo Real janaStill a threat: Shaw and Tyler Blackett keep a close eye on Ronaldo as he dribbles with the ball for Madrid
Shaw na Tyler Blackett wakitafuta mbinu za kumpokonya mpira Ronaldo 
Javier Hernandez ‘Chicharito’ akawafungia Mashetani Wekundu bao la tatu dakika ya 80 mbele ya mashabiki 109,318 waliotapisha Uwanja wa Michigan.
Kikosi cha United kilikuwa; De Gea, Keane, Jones, Evans/Blackett dk45, Valencia/Lingard dk61, Herrera/Cleverley dk45, Fletcher, Young/Shaw dk45, Mata/Kagawa dk61, Welbeck/Zaha dk41 na Rooney/Hernandez dk61.
Real Madrid; Casillas, Arbeloa/Ronaldo dk73, Pepe, Ramos, Fernandez, Alonso/De Tomas dk55, Carvajal, Illarramend, Modric, Bale na Isco.

0 comments: