Wednesday 6 August 2014

LAMPARD AANZA KAZI RASMI MAN CITY... ANGALIA HAPA AKIWA MAZOEZINI

 

KLABU ya MANCHESTER CITY imethibitisha usajili wa kiungo wa zamani wa Chelsea, Frank Lampard kwa mkopo wa miezi sita.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wametangaza habari hiyo leo, na Lampard alifanya mazoezi na timu yake mpya kwa mara ya kwanza baadaye leo. 
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 36 amesajiliwa na klabu dada ya Manchester City, NEW YORK CITY kama mchezaji huru, lakini anarudi England kwa sababu msimu wa Ligi Kuu ya Marekani unaanza mwakani.
Siku ya kwanza: FRANK LAMPARD amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na Manchester City leo baada ya kukamilisha usajili wake wa mkopo kutoka New York City
New colours: The former Chelsea midfielder trains at a wet Carrington with his new Manchester City team-mates
Rangi mpya: Kiungo wa zamani wa CHELSEA amefanya mazoezi Uwanja wa Carrington na wachezaji wenzake wa timu yake mpya, Manchester City

0 comments: