Pamoja na hayo pia wametakiwa Msimu ujao wasizidishe Fungu la Fedha za Mishahara ya Wachezaji wao kupita lilivyo hivi sasa.
Kwenye Faini, City wametakiwa walipe Pauni Milioni 18 tu na nyingine kusimamishwa kuangaliwa mwenendo wao.
Mara baada ya kutangazwa Adhabu hiyo, 
Man City wamemesema wao hawakubaliani na uamuzi huo kwani wanaamini 
hawakukiuka FFP na hivyo watalipeleka mbele suala hili.
Vile vile, City wamesema kwenye Msimu 
huu wa UEFA CHAMPIONZ wao walitumia Wachezaji 21 tu hivyo hiyo Adhabu ya
 kuwabana wasizidishe Wachezaji 21 haitawaathiri sana.
Inaaminika Adhabu hiyo ni sawa na ile 
waliyopewa Paris Saint Germain kwa pia kukiuka FFP kama zilivyotolewa na
 Bodi ya Udhibiti Fedha ya UEFA, CFCB, [Club Financial Control Board].
Chini ya Sheria za FFP, Klabu zinatakiwa zisipate Hasara ya zaidi ya Pauni Milioni 37 katika Misimu miwili iliyopita.
Man City wao wamepata Hasara 
inayokaribia Milioni 149 kwa Misimu miwili iliyopita ikiwa ni Pauni 
Milioni 97 Mwaka 2012 na Pauni Milioni 51.6 kwa Mwaka 2013.
Man City na PSG ni miongoni mwa Klabu 9 
ambazo zimetinga kwa CFCB na kupewa hadi mwishoni mwa Wiki hii kufikia 
makubaliano na UEFA  kuhusu Adhabu zao.
City wakikata Rufaa watasikilizwa na 
Jopo Maalum ambalo uamuzi wake hauna mjadala na upo uwezekano wa 
kuamuliwa Kifungo kwa City kutocheza Ulaya.












0 comments:
Post a Comment