KATIKA
 hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja anayedaiwa kuwa mkazi wa 
wilayani Tarime, mkoani Mara, amemtelekeza mtoto wake kwenye baa mjini 
Bunda na kutokomea kusikojulikana.
Tukio
 hilo lililothibitishwa na jeshi la polisi, limetokea juzi jioni, katika
 baa moja iliyoko mjini Bunda, baada ya mwanamke huyo kufika katika eneo
 hilo na kumnunulia mtoto wake soda na andazi na kisha kuondoka 
akimwacha motto huyo.
Imeelezwa
 kuwa mwanamke huyo alimwacha mtoto wake huyo wa jinsi ya kike, 
ajulikanaye kwa jina la Lusia Mwita, anayekadiliwa kuwa na umri wa kati 
ya miaka mitano hadi sita, pamoja na mfuko wa wa nailoni uliokuwa na 
nguo za mtoto huyo.
Habari
 zaidi zinasema baada ya mtoto huyo kutelekezwa alianza kutangatanga, na
 ndipo akaokotwa kwenye uchochoro na mwanamke mmoja, ajulikanaye kwa 
jina la Pendo Joseph, mkazi wa mtaa wa Kabarimu mjini Bunda, ambaye 
alimpeleka kwenye kituo cha polisi. 
Polisi
 wamesema kuwa baada ya mwanamke huyo kutoa maelezo yake, aliruhusiwa 
kuondoka na mtoto huyo, ambapo sasa anaishi naye akisubiri wazazi wake 
waweze kumchukuwa.
Akizungumza
 kwa taabu mtoto huyo amesema kuwa walipanda ndani ya basi kutoka 
Tarime, ambapo mama yake alimwambia kwamba wanakwenda kwa babu yake 
mjini Bunda, na baada ya kufika kwenye eneo hilo mama yake alimwacha na 
kwenda kusikojulikana.
Na Ahmed Makongo, Bunda
 






 
 
 
 






0 comments:
Post a Comment