Ili
 kuwafikia wananchi wengi, uzinduzi wa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania utakaofanyika kesho, Jumatatu, Juni 3, 2013, 
kuanzia saa 8:00 mchana  katika viwanja vya Karimjee, 
jijini Dar es Salaam utarushwa moja kwa moja na vituo vya TBC1, TBC 
Taifa, ITV, Star TV, Channel Ten, ZBC TV na ZBC Redio. Wadau hawa 
wamekubali kufanya hivyo baada ya kuombwa.
Uzinduzi huo utarushwa moja kwa moja na vituo hivyo kuanzia saa 8:00 mchana. 
Rasimu
 hiyo ya Katiba imetokana na maoni ya wananchi, viongozi na makundi 
mbalimbali waliyowasilisha kwa Tume kupitia njia mbalimbali zikiwemo 
mikutano, barua pepe, ujumbe mfupi wa simu za mikononi (sms) na 
nyinginezo.
 






 
 
 
 






0 comments:
Post a Comment