Monday 26 October 2015

Maalim Seif Sharif Hamad Ajitangazia Ushindi wa Urais Zanzibar..


Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.
   
Aidha, akiongea  na  wanahabari, Maalim Seif Sharif Hamad  ameitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo halisi kama yalivyo kwenye fomu zinazotoka vituoni.

Chanzo:DW Swahili

0 comments: