Wednesday 13 April 2016

Jackie Chandiru wa Blue 3 nae Hoi Kwa Madawa ya Kulevya


Madawa ya kulevya si janga linaloviumizwa vichwa vya wadau wa muziki wa Bongo Flava, bali Uganda pia mambo si mambo.

Muimbaji wa zamani wa kundi la Blue 3, Jackie Chandiru yupo kwenye hali mbaya baada ya kuathirika na utumiaji wa unga. Amekuwa kwenye wakati mgumu zaidi baada ya ndoa yake kuvunjika na sasa yupo rehab huku afya yake ikiwasononesha wengi.

Yupo kwenye kituo cha Bunamwaya ambako madaktari na washauri nasaha wanamsaidia arudi kwenye hali yake ya kawaida. Waliomuona wanadai kuwa hata ngozi yake imeanza kubabuka. Amekuwa akitumia cocaine na madawa mengine.

0 comments: