MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Sunday, 2 June 2013

KUDONDOKA KWA UKUTA WA TANGI LA MAJI LA UAWA WATU 3 LEO PEMBA

   ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuokoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na Ukuta wa tangi la Maji Machomanne Chake Chake Pemba leo
 
 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiutoa mwili wa Marehemu juu ya Mnara wa tangi la Maji Machomanne, ulioangukiwa na ukuta wa tangi hoo



 WANANCHI mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la Maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu leo asubuhi. (picha na Abdi Suleiman


 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiushusha chini mwili wa marehemu aliyepoteza maisha baada ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa Tangi la Maja Machomanne Pemba



 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiupeleka mwili wa marehemu katika gari ya kubebea wagonja, ulioelemewa na ukuta wa mnara wa Tangi la Maji Machomanne Pemba
 WANANCHI mbali mbali wakiwa katika hospitali ya chake chake , wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
 Mkuu wa mkao wa kusini Pemba, Juma Kassim Tindwa, akimfahamisha jambo waziri wa Nnchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed, walipofika katika Hospitali ya Chake Chake, kuaangalia majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo.
DAKTARI bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya chake chake, kufuatia kuwangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la Maji Mchomanne Pemba. 



JUMLA ya watu watatu wamefariki ndunia papo hapo na watatu kujeruhiwa baada yakuangukiwa na ukuta mnara wa tangi la maji uliopo machomanne chake chake pemba, majira ya saa tatu za asubuhi ya leo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Suleiman Hassan Suleima, amesema kuwa, merehemu hao walifikiwa na mauti wakiwa katika kazi ya kuteremsha ukuta wa mnara wa tangi la maji ambao walikuwa wameshaukata.
Kamanda Suleimana alisema kuwa, ukuta huo ulikuwa tayari umeshafanya ufa wa kupasuka, hivyo wakati wakiwa kazini kuuteremsha ukuta huo, ulianguka na kuwaelemea marehemu hao pamoja na mejeruhi waliokuwa juu wakiuteremsha ukuta huo.
Kamanda alisema kuwa idadi ya mafundi waliokuwepo kazini hapo, walikuwa ni watu 12 ambapo watatu wamepoteza maisha papo hapo na watatu kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya chake chake na wengine sita walikimbia na jeshi la polisi liko katika utaratibu wa kuwatafuta kwa ajili ya kuelewa hali zao.

Aliwataja marehemu hao kuwa, ni Juma Rashid Juma (35)mkaazi wa chanjaani, Suleiman Mohammed Abdiadi “maarufu golo” (55) mkaazi wa kwale na Salum Muhidini Vuai “Bandudu” (35) mkaazi Madungu wote ni wakaazi wa wiliya ya chake chake mkoa wa kusini Pemba.
Aliwataja majeruhi kuwa ni Jakson John (26) mzaliwa wa Iringa mkaazi wa msingini, Ali Saleh Ali (35) mkaazi wa michakaeni na Yohana Richerd (25) mkaazi wa machomanne Chake Chake Pemba.
“baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi tulifika katika eneo la tukio na tukashirikiana kikamilifu na wenzetu wa vikosi vya ulinzi na usalama wote wa pemba katika kuokoa maisha ya wananchi wetu waliokuwepo hapo”alisema kaimu kamanda Suleiman.
Aidha aliwataka wananchi kutoa mashirikiano pale panapotokea majanga kama hayo, ili kuweza kuokoa maisha ya wananchi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, DK Hilali Juma Mohammed, wa Hospitali ya Chake Chake, amesema kuwa kati ya marehemu hao watatu, wawili waliumia kichwa, Kifua na Mikono.
Alisema kuwa merehemu Suleiman Mohammed Abdiadi “maarufu golo” aliumia sehemu za kichwa ambacho kilikatika moja kwa moja, Kifua na Mikono, hivyo baada ya kumaliza taratibu za uchunguzi waliweza kuzikabidhi maiti hizo kwa ndugu na Jamaa zao.
“Tulishirikiana kikamilifu na vikosi vya ulinzi na usalama vyote pamoja na uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Kusini Pemba, katika kuwakabidhi miili hiyo kwa jamaa wa marehemu kwa ajili ya Mazishi”alisema Dk Hilali.
Akitoa tamko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mhammed, aliwataka wananchi waliopoteza ndugu zao katika aji ya kuangukiwa na ukuta huo, kuwa na subra katika kipindi hichi kigumu kwao.
Alisema kuwa msiba huo, sio wao pekeyao bali ni wataifa kwa ujumla, hivyo Serikali iko pamoja nao katika msiba huo na itashirikiana nao kwa mazishi na madawa kwa wale ambao wamepata majeruhi na kulazwa katika hospitali.
“Nimepokea habari ya kusikitisha kutoka kwa viongozi wenzangu, kuhusu kuanguka kwa ukuta na kupelekea kupoteza maisha ya wananchi watatu, na wengine watatu kujeruhiwa”alisema Mohammed Aboud.
Kwa upande wake mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Wawi kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohammed, alisema kuwa kukosekana kwa taaluma kwa wananchi juu ya vifaa vitakavyo tumika pamoja na athari zake zitakazo tokea imechangia kutokea kwa tukio hilo.
Alisema kuwa, hilo lililotokea ni funzo tosha kwa serikali na kuitaka serikali kuwa makini wakati wote na kabla ya kufanya kitu chochote waangalie athari yake ili kuweza kuepusha majanga kama hayo.
Aidha alisema kuwa, kutokea kwa tuki hilo ni funzo kwa tasisi zote za umma pale wanapotaka kufanya kitu lazima wajuwe athari yake inayoweza kutokea hapo baadae, ambamba na kuwataka wananchi kuwa watulivu katika kipindi hiki kifupi.
“Nawashukuru sana vikosi vyetu vya Ulinzi licha ya kukosa zana za kisasa, walipopewa taarifa tu wamefika na kuanza kuokoa maisha ya wananchi, hilo ni jambo la kuwapongeza, wananchi tuwe pole katika kipindi hiki kigumu cha msimba kwani ni msiba wetu sote huu.”alisema Hamad Rashid.
Naye mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kassim Tindwa, aliwashukuru wananchi wa maeneo ya Machomanne kwa juhudi zao kubwa walizozionyesha kabla ya kufika kwa vikosi vya uokozi katika tukio hilo.
Aliwataka wataalamu wanaotoa tenda kutumia taaluma zao wakati wanapotoa tenda kwa kuchukuwa wafanya kazi wenyetaaluma, kwa kuangalia wafanyakazi wao taaluma zao wakati wanapotaka kufanyiwa kazi zao.
Aliwapa pole familia zote zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika eneo la tukio hilo, katika kipindi hicho kigumu. “ Sina budi kuwapongeza wananchi wote waliofika katika tukio hilo, na kuweza kusaidia uokozi kabla ya kufika kwa vikosi vya uokozi katika tukio hili”alisema Tindwa.
Kwa upande wake Mkuu wa kikosi cha Zimamzoto na Uokozi Pemba, ACF Iddi Khamis Juma, alisema kuwa katika tuko hilo changamoto kubwa iliyowakabili ni kukosekana kwa vifaa vya kisasa vya uokozi, hali iliyopelekea kuchukuwa muda mwingi kwa kutumia vufaa vya kienyeji.
Alisema kuwa, licha ya kutumika kwa vifaa vya kienyeji lakini waliweza kuziopoa marehemu zilizokuwa zimekwama katika mnara huo, sambamba na kuwataka wananchi pindi likitokea tukio kutoa taarifa kwa wakati muafaka kwa vyombo vya Sheria.
“Tulipopata taarifa tu tuliweza kupeana taarifa makamanda wote na kufika katika eneo la tukio na kuweza kuziopoa maiti zilizokuweko juu ya Mnara huo, ila kikwazo ni zana za uokozi kwani tumetumia dhana duni”alisema.
Naye mmoja kati ya wafanyakazi katika mnara huo, Said Mohammed , alisema kuwa katika kazi hiyo jumla wako vijana 12 ambao ndio wanofanya kazi ya ubomoaji wa mnara huo.
Said alisema kuwa, wanapofika asumuhi huchonga kuta hilo kwa kutumia drili ili kuweza kuliangusha au kuvunja kidogo kidogo, na baadae hushuka chini na kuuvuta kwa gari huo ukuta.
“Leo kabla ya hawajateremka chini, ukuta uliwaangukia na tukaamua kupanda juu kwa lengo kuwaokoa merejeruhi kwanza waliokuwepo hapo juu”alisema kiongozi huo.
Ujenzi huo wa mnara wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba, unaendeshwa na kampuni wa Serengeti Limited ya Tanzania Bara.

 Na Abdi Sueliman Na Bakari Mussa, Pemba.

MBUNGE MSIGWA NA WENZAKE KUFIKISHWA TENA MAHAKAMANI KESHO



 Mbunge  Msigwa akishuka katika gari ya  polisi baada ya kufikishwa mahakamani siku alipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza
 Mbunge  Msigwa akishuka katika gari hilo la polisi tayari kwa kuelekea  chumba cha mahakama
 Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya  kufikishwa mahakamani kwa  mara ya kwanza
 Watuhumiwa  wengine wa vurugu  za machinga  na polisi  wakishuka katika karandinga la polisi
Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa na viongozi  wengine wa Chadema akiwemo katibu mwenezi wa Chadema na diwani wake pamoja na watuhumiwa wengine wa kesi ya vurugu za machinga na polisi kufikishwa mahakamani tena kesho jumatatu

URUSI YAZINGA AZIMIO KUHUSU QUSAIR


 
 Mwanaharakati wa Qusair akitembea katika mji huo unaoshambuliwa na jeshi la serikali ya Rais Assad

Wanabalozi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanasema kuwa Urusi imezinga mswada wa azimio la kueleza wasiwasi kuhusu hali, hasa ya raia, kwenye mji wa Syria wa Qusair ambao umezingirwa.
Mashambulio ya serikali dhidi ya mji huo unaodhibitiwa na wapiganaji yameendelea kwa zaidi ya majuma mawili na wakaazi wamenasa bila ya chakula, maji wala madawa.
Lakini wanabalozi wanasema Urusi haitaunga mkono mswada huo wa azimio kwa sababu Umoja wa Mataifa haukushughulika wakati mji huo ulipotekwa na wapiganaji.
Hapo jana Umoja wa Mataifa na Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu, ICRC, yalitoa maombi kuwa wasaidizi waruhusiwe kuingia Qusair.
Msemaji wa ICRC, Dibeh Fakhir, aliiambia BBC taarifa wanazopata kuhusu hali katika mji huo:
" Ripoti tunazopata zinasema kuna upungufu mkubwa wa maji, chakula na madawa.
Piya zinaeleza kuwa mamia ya raia wamejeruhiwa na hawawezi kupata matibabu.
Maelfu tayari wameshakimbia Qusair na maelfu wanasaidiwa na Shirika la Msalaba Mwekundu la Syria, likisaidiwa na ICRC na mashirika mengine.
Hata hivo inaripotiwa maelfu bado wako ndani ya mji - kati yao ni mamia waliojeruhiwa vibaya lakini haiwezekani kuwatibu"
Alisema kuweza kusaidia inavyotakiwa, ICRC inahitaji kuwepo Qusair bila ya kuingiliwa kati na serikali.

Chanzo bbcswahili

VITA VYA SYRIA VYAZIDI KUTAPAKAA LIBNAN



Wapiganaji wa Libnan wanaosaidia serikali ya Syria wakiwa zamu kwenye mpaka na Syria
 Katika ishara nyengine kuonesha jinsi vita vya Syria vinavoathiri taratibu utulivu katika nchi ya jirani ya Libnan, askari huko wanasema wapiganaji kadha wa Syria waliuwawa Jumamosi usiku katika mapambano na vikundi vya Hezbollah nchini Libnan karibu na mpaka wa Syria.

Inaarifiwa mapigano hayo yalitokea mashariki mwa bonde la Bekaa katika mji wa Baalbek.
Jumamosi makombora na mizinga kadha ilirushwa dhidi ya eneo hilo na makombora zaidi yamepiga piya mitaa ya kusini mwa Beirut.
Wapiganaji wa Syria wamesema watafanya mashambulio ndani ya Libnan kulipiza wapiganaji wa Hezbollah kumsaidia kivita rais wa Syria, Bashar al Assad.

Chanzo bbc

SIMBA NA YANGA HATARINI KUSHIKIRI KOMBE LA KAGAME DARFUR



 
clip_image002
Siku kadhaa baada ya Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati - CECAFA kuidhinisha michuano ya kombe la Kagame kuchezwa mjini Darfur -Sudan, serikali ya Tanzania imetoa tamko kuhusu timu za Simba na Yanga kwenda kushiriki michuano hiyo huko Sudan kwenye eneo ambalo limekuwa likiandamwa na vurugu kwa miaka kadhaa sasa.
Kwa mujibu wa msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga ni kwamba serikali haidhani ni busara kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenda kwenye eneo hilo kushiriki Kagame Cup kutokana hali mbaya ya usalama iliyopo Darfur.
HIVI NDIVYO ALIVYOANDIKA KAMWAGA KWENYE UKURASA WAKE WA FACEBOOK.
Ezekiel Kamwaga
Breaking News...... Serikali imesema haioni busara ya Kagame Cup kupigwa Darfur.... Hakuna hoteli ya maana na watu wanashauriwa kutembea na fulana zinazozuia risasi kupenya... Nadhani hii ndiyo stori kubwa ya kimichezo kwa leo.... Je, mnadhani itakuwa busara kwa Simba na Yanga kushiriki?

KIBAKA ACHOMWA MOTO JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 

clip_image003
Jamaa huyu asie na roho ya huruma akimmalizia mtuhumiwa na bonge la tofali! Tukio hili limetokea maeneo ya mbagala charambe mida ya saa sita mchana baada ya kibaka huyu kubahatika kukuta raia mwema kasahau kufunga mlango, Kibaka akazama ndani na kuchukua begi languo taratiiibu kama lake! Hakuridhika na begi alivyotazama pembeni akaona simu akaihifadhi mfukoni kiaina! Ile kutokanje tu akakutana na wenye nyumba uso kwa uso!!!
Hapo ndipo mbio za marathon zilipoanza!!!!! Watu mwiziii mwiziiii mwiziiiiii mwiziiiiiiiiii!!!!! Jamaa akabahtika kujisweka kwenye jumba bovu lililoko uchochoroni na kuinusuru roho yake, Raia wenye hasira kali hawakumuona wakapita, Kufika mbele kidogo wakajadiliana na kukata tamaa wakati wakirudi majumbani kwao mara ghafla! Kurupu! Jamaa akachomoza kwenye dirisha la lile jengo bovu alilojificha, Harakati zikaanza upyaaaaaa!!!!! Aaaa... Anko jambazi hakuchukua raundi akatiwa mikononi.
clip_image003[6]Anko jambazi ameveshwa tairi na kutiwa moto! Izraeli anapiga push up pembeni!!!clip_image003[8]

MWILI WA NGWAIR KUTOWASILI TENA LEO HII




Kamati ya msiba ya mwanamuziki Albert Mangwea, imeleta taarifa kwamba mwili wa Ndugu  yetu Albert Mangwea hautoweza kufika siku ya jumapili ya tarehe 2/ 06/2013 kama ilivyo taarifa hapo awali, hii ni kutokana na sababu  zilizokuwa nje ya uwezo wetu.
Kwa sasa tunasubiri taarifa kamili kutoka kwa wenzetu/wawakilishi  wetu waliopo nchini Afrika Kusini, mara tutakapopata taarifa hizo  tutawafahamisha zaidi.
Tunaomba radhi watanzania wote kwa usumbufu wote  uliojitokeza  tushirikiane na uvumilivu kwa hili.

UHAMIAJI WALIOSHUGHULIKIA SUALA LA KABENDERA WACHUKULIWE HATUA

KAMATI iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Emmanuel Nchimbi kuchunguza tukio la kusumbuliwa kwa wazazi wa mwandishi wa habari Erick Kabendera na maofisa Uhamiaji imependekeza maofisa hao wachukuliwe hatua stahiki za kinidhamu kwani walikiuka taratibu za kazi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Augustine Shio akisoma taarifa ya kamati hiyo jana mbele ya waandishi wa habari, alisema maofisa Uhamiaji waliochunguza uraia wa Erick na wazazi wake hawakuwa makini katika kazi yao.

Shio alisema kitendo cha kukosa umakini kilisababisha malalamiko kutoka familia ya Erick, wazazi wake pamoja na vyombo vya habari.

Aliongeza kuwa uraia wa Erick, baba yake mzazi Nolosco Kabendera na mama yake Verdiana Mujwahuzi haubishaniwi kuwa wote ni raia wa Tanzania wa kuzaliwa.

Lakini kamati hiyo imejiridhisha kwamba zipo kasoro za msingi za jina zilizobainika katika mchakato wa maombi ya pasipoti ya Erick iliyotolewa mwaka 2006 ambazo zilisababisha Idara ya Uhamiaji kufanya uchunguzi ili kuthibitisha taarifa za maombi hususani uraia wa mwombaji.

“Pia tumebaini kwamba Reginald Mengi hajahusika kwa namna yoyote na mchakato wa uchunguzi wa uraia wa Erick Kabendera na kuhojiwa kwa wazazi wake na Idara ya Uhamiaji,” alisema Shio ambaye ni Mkurugenzi wa Malalamiko katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Nchimbi aliunda kamati hiyo ya watu watatu Machi mwaka huu baada ya kuombwa na Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Idara ya Habari (Maelezo) na Jukwaa la Wahariri kuchunguza na kutafuta suluhisho la kuwepo matukio kadhaa ya uhalifu dhidi ya waandishi wa habari hapa nchini.

Katika mkutano wake na vyombo hivyo, mambo mbalimbali yaliwasilishwa lakini tukio moja la kusumbuliwa kwa wazazi wa Erick Kabendera kwa madai kuwa si raia wa Tanzania liliombwa lichunguzwe kwa maelezo kuwa kuna taarifa zisizotiliwa shaka na za kuamini kwamba watumishi wa Uhamiaji waliotumika walilipwa fedha ambazo hazikutoka katika mfumo rasmi wa Serikali bali zilitolewa na mtu mmoja zikapitia kwa ofisa wa Ikulu kwenda Uhamiaji.

Licha ya Moat, wengine ambao walilalamikia suala hilo ni waandishi wasio na mipaka pamoja na Erick mwenyewe ambao kwa nyakati tofauti waliandika barua kwenda kwa Waziri kulalamikia hatua hiyo ya Uhamiaji.

Barua hizo zilionesha kumhusisha Mwenyekiti wa MOAT, Reginald Mengi na tukio hilo hasa baada ya Erick kutoa ushahidi katika shauri la Mengi dhidi ya Sarah Hermitage katika Mahakama Kuu London, Uingereza.

Kamati hiyo pamoja na Shio, wengine walioteuliwa kwenye kamati hiyo ni Mligo Mussa kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali na Felix Wandwe mjumbe kutoka ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU).

---
Imenukuliwa kutoka HabariLeo


Saturday, 1 June 2013

MWANAMKE MMOJA ANUSURIKA KUCHINJWA

 

Mwanamke Mery Mbosa anayeishi kama mkimbizi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake.
========================================

Na Gustav Chahe, Iringa


MAMA mmoja mkazi wa Itunundu – Pawaga katika Mkoa wa Iringa Mery Mbosa anaishi kama digidigi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake na kulazimika kuhama kijiji kwa ajili ya kunusuru maisha.

Akiongea na mtandao huu jana, Bi Mbosa alisema maisha yake yapo hatarini kutokana na kuvamiwa na mtalaka wake mara kadhaa akiwa nyumbani na kumuumiza.

Alisema alilazimika kutalakiana baada ya mwanamume huyo kuwa mkorofi kiasi cha kupigwa, kutokuwa huru kutumia mazao ambayo walilima wote na hata kutokuwa huru kuongea na watu hata kama ni ndugu zake kwa madai kuwa ni wivu wa kimapenzi.

Alisema mtalaka wake amegeuka kuwa mnyama na kufika nyumbani kwake usiku wa manane na pindi anapokuta mlango umefungwa huanza kurusha mawe madirishani huku akitaka kuvunja mlango ili kuingia kumdhuru.

Amemtaja mtalaka wake kuwa ni Phabiani Msilamgunda ambaye miezi ya hivi karibuni alikutana na ye njiani akielekea shambani akamvamia akiwa na kisu kwa kutaka kumchinja na kuokolewa na watu ambao walikuwa jirani.

“Ilikuwa 23 Machi mwaka huu nilikuwa nikielekea shambani nikakutana na mtalaka wangu akiwa na kisu mkononi akanivamia huku akisema nakuchinja laeo lakini kwa bahati nzuri kulikuwa na watu jirani wakaniokoa vinginevyo ningekuwa marehemu.

“Lakini hata hivyo amekuwa akimtukana hata mama yangu mzazi (mama mkwe) akitaka kupiga pia na kila wakati nimekuwa nikishtaki hadi ofisi zinanichoka pamoja na kuwa ninapokelewa na akiitwa haendi kwa sababu amekuwa mbabe” alisema bi Mbosa.

Hata hivyo Mbosa alisema kuwa aliwahi kupigwa na kuumizwa vibaya na kulazimika kushtaki mahakamani japo kuwa hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki na kuhatarisha zaidi maisha yake.

“Nilipigwa na kuumizwa vibaya kesi ikapelekwa mahakamani lakini hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki kwangu na baada ya hukumu maisha yangu yamekuwa ni ya hatari zaidi” alisema.

Kwa mujibu wa maelezo ya wananchi wa kijiji hicho ambao wameeleza kushuhudia mama huyo akinusurika kuuawa na jinsi maisha yake yanavyozidi kuwa mabaya, walisema kiburi cha Msilamgunda kinatokana na dada yake ambaye ni diwani wa viti maalum (CCM).

Gazeti hili limebaini kesi ambayo mama huyo hajaridhika na hukumu ni Jinai No. 22/2013, mshitakiwa Phabiani Msilamgunda ambayo ilitolewa hukumu Mei 21 Mwaka huu.

Imeelezwa kuwa katika utoaji huku hiyo hakimu aliyetajwa kwa jina moja la Masuwe alimtaka mtuhumiwa alipoe faini ya shilingi laki mbili pamoja na gharama ya kesi shilingi 45 elfu jambo ambalo lilifanyika hivyo na mtuhuhumiwa kuwa huru kwa vitisho kuwa lazima ammalize mwanamke huyo.

Pamoja na kutokuridhika na hukumu iliyotolewa, Mkuu wa kituo cha Polisi cha Pawaga Fedrick Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mama huyo na kuiomba serikali kumsaidia ili aishi kama wanavyoishi wananchi wengine.

Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mwanamke huyo mbegu ya mpunga na kumfanya kuwa mtumwa kwa kukosa chakula bila kujua hatima ya maisha yake.

“Baada ya hukumu nilikwenda shambani nilikokuwa ninaanda mbegu ya mpunga kwa ajili ya kupanda nikakuta watu wananing’oa, nilipouliza walisema wametumwa na Mkuu wa kituo cha polisi. Hivi sasa naishi kama ndege jamani sijui nitakula nini kwa sababu hata mashamba niliyokuwa nalima nilinyang’anywa na mbegu niliyokuwa nimeandaa kwa ajili ya kupanda polisi wameninyang’anya” alisema.

Alipotafutwa kwa njia ya simu kwa ajili ya kutolea maelezo, Veronica Msilamgunda ambaye ni ndugu na Phabian Msilamgunda alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa yupo kwenye mkutano.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Joseph Malinga alipotafutwa kwa ajili ya ufafanuzi Alikiri kuwa mama huyo ni mhanga mkubwa na anaishi kama mkimbizi kwa hofu ya kuuawa.

“Nalijua sana hilo na ninashukuru kwa kuwa umenitafuta ili nikueleze. Maisha ya huyo mama hatuji yataishia wapi kwa sababu hali ilivyo kwa sasa ni ngumu na anaishi kama mkimbizi.

“Hata akiwa sehemu yenye ulinzi anaona kama hakuna ulinzi kwa sababu ya kile anchofanyiwa. Kiujumla hata sisi viongozi wa kijiji tunaishi kwa mashaka kwa sababu tunatishiwa kuuawa tunapotaka kutafutas suluhu ya huyo mama. Huyu mwanaume tunashindwea kuelewa kama ni mtu wa kawaida maana amegeuka kuwa kamas samba” alismea Malinga.

Hata hivyo alisema anaomba kwa watu wanaoweza kumsaidia mama huyo kupata hifadhi ili aondokane na maisha ya kuishi kama digidigi kule kijijini.
 Na Gustav Chahe, Iringa
Kwa msaada waFrancisgodwinblog

AL-QAEDA WANA SILAHA ZA KIKEMIKALI IRAQ


Al-Qaeda piya inashutumiwa kuhusika na miripuko wa mabomu Iraq

Wakuu wa Iraq wanasema wamegundua njama ya al-Qaeda kutaka kutumia silaha za kemikali nchini Iraq na kuzisafirisha kwa magendo hadi Ulaya na Marekani.

Msemaji wa wizara ya ulinzi, Mohammad al-Askari, alisema idara ya usalama ya jeshi imegundua karakana tatu za kutengeneza kemikali hizo, pamoja na kemikali ya kuharibu neva.
Bwana al-Askari aliiambia televisheni ya Iraq kwamba wanaume watano walikamatwa baada ya kuchunguzwa kwa miezi mitatu.
Wote walikiri makosa, alisema.

POLISI WAONDOKA MEDANI YA TAKSIM

 

Maandamano katika medani Taksim, Istanbul
Baada ya mapambano ya siku mbili na waandamanaji, polisi wameondoka katika medani ya Taksim mjini Istanbul na maelfu ya waandamanaji wameikalia medani hiyo.
      Hapo awali waziri mkuu wa Uturuki, Reccep Tayyip Erdogan, alitoa wito watu waache kuandamana haraka - maandamano makubwa kabisa kwa miaka kadha. Lakini Bwana Erdogan ameahidi kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba polisi walitumia nguvu nyingi.
Nchi kadha zimeeleza wasiwasi kuhusu swala hilo.
Chanzo cha maandamano ni mpango wa kujenga maduka katika medani ya Taksim - mpango ambao Bwana Erdogan anasema atautekeleza.
        Waandamanaji vijana piya wanailaumu serikali kwamba imekuwa ya kimabavu na kuifanya nchi kufuata Uislamu.
Msemaji wa serikali alikanusha malalamiko hayo alipohojiwa na BBC na alisema tuhuma zenyewe ni za kushangaza.

Chanzo bbcswahili

CWT YASISITIZA MGOGORO WAKE NA SERIKALI BADO MBINCHI


Rais wa CWT Gration Mukoba
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimesema mgogoro kati yake na serikali bado uko pale pale kwa kuwa hawajafikia muafaka wa mazungumzo yao.

Chama hicho ambacho kinaidai serikali zaidi ya sh. bilioni 25, kimeeleza kuwa mbali ya kuwepo kwa vikao kadhaa kati ya chama hicho, lakini hakuna muafaka uliofikiwa.


Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Rais wa CWT Gration Mukoba, alisema amelazimika kuyasema hayo ili wabunge waelewe kabla ya bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haijasomwa Bungeni wiki ijayo.


“Mgogoro wa walimu na serikali umepoa kwa muda tu. Wajue ngoma ya walimu na serikali bado ni mbichi. Hatujafikia muafaka…” alisema Mukoba.


Rais Mukoba alisema wapo walimu waliopanda madaraja muda mrefu, lakini hadi sasa mshahara wanaopata ni wa zamani.


Kwa mujibu wa Mukoba, maamuzi ya nini CWT itafanya yatatolewa mwezi ujao baada ya Baraza la Walimu kukutana.


Alisema hata nyongeza ya mishahara iliyotangazwa na serikali, haihusiani na madai yao.

Akizungumzia mkutano wa mwisho ulioitishwa na Baraza la Majadiliano kati ya Mei 24 na 25 mwaka huu, Rais wa CWT alisema, CWT iliomba serikali kuwapandishia mshahara walimu kwa asilimia 100 lakini serikali ilipinga.

“CWT ilishuka kutoka asilimia 100 hadi 65 wakati serikali ilipanda kutoka asilimia 12.09 hadi 24.19. Baada ya kufikia asilimia 24.19 serikali iliripoti kuwa uwezo waliopewa wa kujadiliana (Mandate) ulikuwa umeisha wakati CWT walikuwa bado wanauwezo wa kuendelea na mjadala kulingana na ‘Mandate’ waliyokuwa wamepewa,” alisema.


Alisema kutokana na hali hiyo, wajumbe wa serikali waliomba muda wa kwenda kujadiliana na wakubwa wao waliowatuma.


CWT mwezi Mei mwaka jana ilitangaza mgomo ambao Mukoba alisema hauku zaa matunda kwani serikali ilikimbilia mahakamani.


Alisema mahakama iliusitisha ambapo pamoja na mambo mengine iliagiza CWT na Serikali kukutana kwenye meza ya mazungumzo.


Baadhi ya madai ya msingi ya walimu ni ongezeko la mishahara kwa asilimia 100, kurudishwa kwa posho ya kufundishia (Walimu wa sayansi asilimi 55 na wa sanaa asilimia 50) na posho ya asilimia 30 kwa walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu.


Alisisitiza kwamba ni ukweli usiopingika kuwa kufufua mioyo hiyo kutafufua utendaji wao na hivyo kuboresha elimu ya Tanzania kwa maslahi ya sasa na baadaye.




 
SOURCE: NIPASHE

: MWALIMU KORTINI KWA KUMWEKA UNYUMBA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI




http://1.bp.blogspot.com/-nknbe6JQTyk/T2-ihTNOqEI/AAAAAAAAAj0/RZFkC-HsqAE/s400/Police1.jpgJESHI la Polisi mkoani Rukwa linamshikilia Mwalimu  Ased Job (31) kwa  kumtorosha  mwanafunzi  wa  kike mwenye umri wa miaka 17  kisha kuishi naye kinyumba kwa zaidi ya miezi  miwili sasa.

Mwalimu  huyo  ambaye  anafanya  kazi  katika Idara  ya Elimu  katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga  anatuhumiwa kuishi  na  mwanafunzi  huyo  anayesoma  kidato  cha pili  kama  mkewe  kwa kipindi  hicho  chote.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Peter Ngusa,  akithibitisha kutokea kwa tukio hilo alisema lilitokea  Februari  mwaka  huu  baada ya mtuhumiwa kumtorosha  mwanafunzi  huyo na kumpeleka  mkoani Mbeya kisha kufanya taratibu za uhamisho kwa lengo la kumhamishia mkoani Mbeya ili akaishi naye huko.

“Baada ya kukamilisha uhamisho  huo mwanafunzi huyo alihamia mkoani Mbeya kisha akaanza kuishi  na mwalimu  huyo  kinyumba  hadi  mwisho  mwa  Mei  mwaka huu  alipomrejesha  mjini  Sumbawanga  na kuendelea  kuishi  naye kinyumba kisha baadaye kukamatwa,” alisema.

Kwa  mujibu  wa  Ngusa kukamatwa  kwa  mtuhumiwa huyo  kunatokana na taarifa za siri  za  wasamaria  wema  na kwamba anatarajiwa kufikishwa  mahakamani  muda  wowote  mara baada ya  ya upelelezi  wa  awali  dhidi  ya shauri  lake kukamilika.
CHANZO: TANZNAIA DAIMA

UTAFITI WA MADINI YA CHUMA, LIGANGA-NJOMBE WALETA MATUMAINI

 



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kulia) akionyeshwa sampuli mbalimbali za madini ya chuma kwenye kituo kinachofanya utafiti wa awali kuhusu kiwango cha chuma kinachoweza kupatikana kwa kuchimbwa eneo la Liganga, wilayani Ludewa mkoani Njombe alipotembelea karakana ya kampuni ya Kichina ya Tanzania China International Mineral Resorce Ltd, inayofanya uchunguzi huo. Anayempa maelezo ni  Meneja Utawala wa kampuni hiyo, Tao Jian. Kushoto ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
 
Tao Jian akiwaonyesha Kinana na msafara wake, ramani linalofanyiwa kazi na kampuni yake katika kutafiti aina na kiasi cha Chuma kitakachoweza kupatikana Liganga
 
Mabosi wa Kampuni ya Kichina inayofanya utafiti wa aina na kiasi cha chuma kitakachopatikana Liganga, wakitoa maelezo ya jumla kuhusu mradi huo unavyoendelea.
 
Kilima cha madini ya Chuma, kinavyoonekana kwa mbali eneo la Liganga
 
 

MWILI WA MSANII NGWEA KUWASILI KESHO JUMAPILI



MWILI wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, marehemu Albert Mangwea ‘Ngwair’ sasa unatarajiwa kuwasili nchini kesho badala ya leo kama ilivyotaarifiwa awali.M
 http://1.bp.blogspot.com/-6w6OrnTpMqY/UadLwEH2bXI/AAAAAAAACJE/Sj2S5Yk3YSM/s1600/579495_275410252604430_1485125168_n.jpg
Kwa mujibu wa taarifa ya kamati ya mipango ya mazishi ya msanii huyo iliyotolewa jana inayoongozwa na Kaka wa marehemu, Kenneth Mangwea, mwili huo utawasili Jumapili majira ya saa 8, mchana na kisha kufuata taratibu zingine.

“Mwili utafika nchini siku ya Jumapili majira ya saa nane mchana na sio Jumamosi (leo), kama ilivyotaarifiwa hapo awali,” ilieleza taarifa hiyo.

Sababu za mabadiliko hayo, imeelezwa ni kutokana na Watanzania waishio Afrika Kusini, kuomba kutoa heshima za mwisho, Jumapili.

Kwa hatua hiyo, kamati ilibainisha kuwa kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani, watapata nafasi ya kuuaga mwili Jumatatu majira ya saa 2 asubuhi hadi 6 mchana na baada ya hapo, wataelekea Morogoro kwa ajili ya mazishi, Jumanne.

Aidha, kamati iliomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza, huku ikiomba wadau kuendelea kuwaombea kufanikisha salama shughuli hizo za mazishi

WABUNGE WA CHADEMA NA CUF WAKUBALI KUOMBANA LADHI

Dodoma. Vyama vya CUF na Chadema vimekubali kuombana radhi ili mgogoro baina yao uishe baada ya misimamo ya pande zote kuvunja kikao cha Bunge mara mbili, juzi.
Kutokana na maridhiano hayo, Bunge leo litaendelea na mjadala wa makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, baada ya kukwamishwa mara mbili na mzozo huo.
Mzozo huo ulizuka baada ya hotuba iliyoandaliwa na Chadema na kusomwa na Msemaji wa Kambi ya Upinzani Bungeni wa wizara hiyo, Ezekiel Wenje kudai kuwa CUF inafuata itikadi za Kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake mikuu ni kupigania haki za ndoa za jinsia moja yaani ‘usagaji’ na ‘ushoga’.
Vyama hivyo vyote viliombana radhi bungeni ili kumaliza mzozo huo, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kuamuru pande zote kufanya hivyo kulingana na ushauri wa Kamati ya Maadili ya Bunge.
Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliomba radhi kwa upande wa Chadema, wakati upande wa CUF aliomba Mnadhimu Mkuu wa chama hicho Bungeni, Rashid ally Abdalah.
Pamoja na maombi hayo ya msamaha, pande zote ziliendelea kusimamia misimamo yao, lakini wakasema wanazingatia masilahi ya taifa kwa kuombana radhi ili Bunge liendelee kujadili bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje.
Kuhusu kuihusisha CUF na sera zilizotajwa na kuleta tafrani, Mbowe alisema: “Yapo mengi ya (wabunge) kuyajadili. Hili (la ushoga na usagaji) siyo muhimu. Yapo mengi yenye masilahi kwa taifa. Bunge limeahirishwa pasipo sababu ya msingi,” alisema Mbowe na kuomba radhi.
Abdalah alikiri kuwa kauli ya Chadema ilizua mtafaruku na hasira kwa wabunge wa Chama chake na hata kujikuta wakifanya mambo ambayo ni kinyume na taratibu.
“Damu ilichemka na kusababisha kutoa maneno ambayo hayafai Bungeni. Naomba radhi kwa hayo,” alisema Abdalah.
Kuomba radhi huko kulitokana na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Bunge, John Chiligati kueleza kuwa baada ya kuzungumza na pande zote pamoja na kufuata ushauri wa wabunge mbalimbali walibaini pande zote zina makosa.
Chiligati alisema katika mahojiano, CUF ilikiri kuwa inafuata sera za Kiliberali lakini siyo zote ikiwamo hiyo ya ushoga na usagaji, hasa ikizingatiwa kuwa Tanzania haikubaliani na tabia ya namna hiyo.
Kwa sababu hiyo, Chiligati alisema Chadema itaomba radhi baada ya kubainika kufanya makosa mawili wakati CUF itaomba radhi kwa vipengele vya makosa manne.

KIGOGO WA CUF UTATANI KWA UCHOCHEZI VURUGU ZA MTWARA

Jeshi la Polisi nchini linadaiwa kumkamata Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha CUF, Katani Ahmed Katani jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za uchochezi na kumsafirisha kwa ndege kwenda mkoani Mtwara.
Habari zilizolifikia Mwananchi Jumamosi na kuthibitishwa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro zilieleza kuwa Katani alikamatwa juzi mchana baada ya kupigiwa simu na maofisa wa polisi wa Kituo Kikuu cha Polisi jijini humo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipoulizwa juu ya kukamatwa kwa kiongozi huyo alisema hana taarifa huku akiomba apewe muda ili aulize.
“Sina taarifa ngoja niulize”, alisema kwa kifupi na hata alipotafutwa baadaye hakupokea simu yake ya mkononi.
“Alipigiwa simu juzi na maofisa wa polisi na kuelezwa kuwa anahitajika kituoni hapo, lakini alipofika alikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi” zilieleza habari hizo na kuongeza;
“Alihojiwa kwa saa kadhaa na jana asubuhi alisafirishwa kwa ndege kupelekwa mkoani Mtwara. Walitaka kumsafirisha kwa basi lakini viongozi wa CUF walikataa jambo hilo, hivyo kulazimika kusafirishwa kwa ndege.”
Habari hizo zilifafanua kwamba kwamba sababu kubwa ya kukamatwa kwa Katani ni kuhusishwa na vurugu zilizotokea mkoani Mtwara kati ya wananchi wanaopinga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda Dar es Salaam dhidi ya polisi.
Kwa upande wake Mtatiro alisema kuwa CUF hivi sasa inajipanga kuweka mawakili kabambe kwa ajili ya kumtetea kiongozi huyo wa vijana wa chama hicho.
“Tulijua tu kuna kiongozi wa chama atakamatwa maana kwa muda mrefu Polisi wamekuwa wakisema kuwa watawakamata viongozi wa juu wa chama. Kwa sasa Katani yupo Mtwara na sababu ya kukamatwa kwake ni kutuhumiwa kuchochea vurugu za Mtwara” alisema Mtatiro.


kwa msaada wananchi gazeti juni 1

KITUO CHA MABASI BOMA NG'OMBE KIMEFUNGWA KWA MUDA

  Kituo kikuu cha mabasi cha wilaya ya Hai kilichopo katika mji wa Boma Ng'ombe kimefungwa kwa muda  ili kupisha matengenezo makubwa ya kuweka lami.

Mkuu wa wilaya ya Hai, Novatus Makunga amewaeleza waandishi wa habari kwamba matengenezo hayo yanayokana na ahadi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010.

Ameeleza kuwa matengenezo hayo ya kipande cha urefu wa kilometa 0.85 utachukuwa siku 45 kwa gharama
 ya shilingi milioni 90.

Amefafanua kwamba matengenezo hayo yataunganisha barabara inayoingia kituoni hapo na ile ya Moshi hadi Arusha pamoja na kukiwekea lami.

Makunga ameeleza kuwa wakati kituo hicho kikiwa kimefungwa, hivi sasa kinatumika kituo cha muda katika eneo la Double Road. Ameeleza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2012/2013, Halmashauri ya wilaya ya Hai ilitengewa jumla ya shilingi 460,810,000 katika mfuko wa barabara.

Wilaya ya Hai ina barabara zenye urefu wa kilometa 466.2 ambapo kati ya hizo, kilomeya 32 ni barabara kuu, kilometa 42 ni za mkoa, kilometa 175.93 ni za wilaya na kilometa 150.27 ni za vijiji na barabara za Hai ni kilometa 66. Amesema kuwa barabara zinazopitika nyakati zote ni kilometa 235.53 ambazo ni sawa na asilimia 50.82.
 


 

WANAFUNZI UWELENI PEMBASEKONDARI WACHAGAWA NA MASHETANI

  -- UONGOZI wa skuli ya sekondari ya Uweleni Pemba, umelazimika kuwazuiya wanafunzi wote wasiende skuli kwa siku ya pili sasa baada ya wanafunzi kuendelea kuchangawa mashetani.

Vituko hivyo vinajiri baada ya skuli hiyo kufanyiwa ukarabati mkubwa na tokea wanafunzi waanze kuyatumia madarasa ‘mapya’ wamekuwa wakikumbwa na mkasa huo na kusababisha tafrani kubwa kiasi kwamba walimu wanashindwa kufundisha kwa utulivu.

Juzi Jumatano (jana), uongozi wa skuli ulilazimika kuwarejesha makwao, wanafunzi wote baada ya hali ya hali kuwa mbaya huku wanafunzi wakianguka na kupiga kelele hovyo huku wengine wakitimua mbio.

Kutokana na tafrani hiyo, Kamati ya Uongozi ya skuli hiyo ilikutana na wazazi wa wanafunzi jioni ya juzi na 


kuamua wanafunzi hao waendelee kubaki majumbani mwao huku ufumbuzi wa kadhia hiyo ukitafutwa.

Baadhi ya wazazi na wanafunzi wa skuli hiyo, wameihusisha hali hiyo na imani za kishirikina, ambapo wamesema kabla ya kufunguliwa tena skuli, ilibidi kutolewe kafara kwa kuchinjwa ngo’mbe.

Hata hivyo kuna tetesi kuwa, matukio hayo yana mkono wa baadhi ya wananchi, ambao walitaka kabla ya skuli hiyo kufunguliwa achinjwe ng’ombe kwanza kitendo ambacho hakikufanyika.

Mwenyekiti wa kamati ya skuli hiyo, Maalim Hemad Ali alisema hali ya wanafunzi kuchagawa iliyojitokeza skulini hapo ni ya kutisha na inaweza kuhatarisha maisha ya wanafunzi, walimu na skuli kwa ujumla.

“Hali ni ngumu, wanafunzi wanapiga makelele ya kutisha, wanajirusha na kujipiga na chini na wengine kufikia hadi kuvua nguo,” alisema kwa huzuni .

Mmoja ya wazazi wa wanafunzi, Kassim Muhammed alitoa ushauri kwa kamati ya skuli na wazazi wenzake kuanzishwa kamati maalum ya wazee wa vijiji wanavyotoka wanafunzi ili kutafutwa undani wa tatizo hilo na kupatiwa ufumbuzi.

Alisema kuundwa kwa kamati hiyo kutarahisisha kuelewa kwa urahisi chanzo cha tatizo na kulipatia ufumbuzi.

Naye Ali Abas Omar alisema isicheleweshwe kutafutwa ufumbuzi kwani wanafunzi wanakosa masomo hali inayoweza kuwaweka katika mazingira mabaya.

Rais wa serikali ya wanafunzi wa skuli hiyo, Nizar Fesal alisema tatizo la kuchagawa linarejesha nyuma maendeleo ya skuli na wanafunzi kwani wanakosa vipindi vya masomo.

Nae mwanafunzi Fatma Salum, ameishauri jamii kujali maendeleo ya watoto wao na kuachana na masuala ya kishirikina.

Alisema jamii haina budi kufurahia ukarabati wa skuli hiyo badala ya kuchukia na kuanza kuwadhuru wanafunzi.
 habari na
  Habiba Zarali, Pemba (  ZanziNews blog)