Monday 2 September 2013

UMOJA WA AFRIKA WATAFUTA SULUHISHO LA KIDIPLOMASIA DRC KWA MAPIGANO MAKALI YANAYO ENDELEA NCHINI HUMO

PictureMary Robinson
Imeandikwa na Mwandishi Maalum — Kufuatia  kurejea tena kwa mapigano makali yaliyotokea wiki iliyopita kati ya majeshi  ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo  (FARD) yakisaidiwa na Jeshi la MONUSCO na kundi la waasi  la M23. Umoja wa Mataifa sasa  unajaribu kutafuta suluhu ya kidiplomasia inayolenga katika kujaribu  kuweka sawa hali ya mambo.

Mapingano  hayo ambayo  siyo tu  yanasadikiwa kuliondoa kundi la M23 katika ngome yake ya vilima vya Kibati Magharibi ya Kivu yamelaaniwa vikali na Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu Ban ki  Moon hasa baada ya kundi hilo la M23 kusababisha  kifo cha  mwanajeshi Mtanzania na kujeruhi wengine kumi wakiwamo wanajeshi  kutoka Afrika ya Kusini.

Mchakato huo wa   kisiasa  unafanywa  na Mjumbe Maalum  wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Kanda ya Maziwa Makuu, Bi. Mary  Robinson, ambaye amewasili katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku ya  jumapili na kutoa  rambirambi zake kwa wahanga wa  mapigano hayo.

Source: kwa habari zaidi www.wavuti.com

0 comments: