MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Sunday, 11 January 2015

EPL: SOTON WAVUNJA REKODI YA MIAKA 27 DHIDI YA MANCHESTER UNITED


Ligi kuu ya Uingereza imeendelea tena jioni ya leo kwa michezo miwili kucheza katika viwanja tofauti nchini humo – moja ya mechi ilikuwa inawakutanisha timu zinazogombania kuendelea kuwemo kwenye 4 bora – Man United vs Southampton.
Mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa Old Trafford umeshuhudia rekodi ya miaka 27 ya Soton kutokuifunga Man United katika uwanja wa nyumbani kwenye EPL ikivunjika.
Goli la dakika ya 69 la Tadic limewapa Southampton ushindi ambao pia umewapandisha mpaka nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi.
Katika mchezo mwingine wa leo hii Arsenal waliifunga Stoke City 3-0 na kupanda hadi nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi.

SERIKALI YATOA SHILLINGI MILLIONI 21 MIKOPO KWA AJIRI YA VIJANA

Serikali imewataka vijana kuitumia vyema mikopo wanayopata katika kuteketeza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ili kujikwamua kiuchumi.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa  Ufutiliaji na Tathimini  toka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Bi.Verdiana Mushi wakati alipotembelea Ofisi ya Halmashauri ya Nzega na kwa ajili ya kukabidhi hundi ya kiasi cha shilingi milioni 21 itakayosaidia kukopesha vikundi vya vijana walioko chini ya Vijana Saccoss Nzega.
“Serikali inaendelea kutekeleza ahadi yake ya kuwasaidia vijana kujikwamua kiuchumi kwa kuwapatia mikopo ambayo itawasaidia kutekeleza miradi mbalimbali ambayo itawaongezea kipato na kuwaondolea umasikini kwani vijana ndiyo nguvu kazi ya nchi” Alisema Bi.Mushi.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nzega Bw. Abrahaman Mndeme ameishukuru serikali kwa kuwapatia mkopo huo vijana wa Nzega kwani kwa kupitia mkopo huo vijana watafaidika sana na pia watachangia kukua kwa pato la Halmashauri na kupunguza vijana wanaoka vijiweni na kushauriana mambo yasiyo na maendeleo katika jamii.
PIX 2
Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Nzega Bw. Abrahaman Mndeme akipokea  barua pamoja na hundi zenye jumla kiasi cha shilingi millioni 21 kutoka kwa  Afisa Vijana wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni  na Michezo hivi karibuni.
“Uongozi wa Halmashauri kwa kushirikiana na Saccoss ya Vijana Nzega utasimamia gawio la fedha hizo kwa vikundi husika na kuhakikisha miradi iliyoandikwa na vikundi hivyo inatekelezwa, pamoja na kufuatilia urejeshwaji mikopo hiyo kwa wakati ili vikundi vingine viendelee kunufaika na mikopo hiyo inayotolewa na serikali”,alisema Bw.Mndeme
Akitoa hamasa kwa vijana Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Bw.Eliakim Mtawa aliwaasa Vijana kuunda vikundi na kujiunga katika Saccoss za Vijana zilizopo katika halmashauri zao ili waweze kuomba mkopo  utakao wasaidia kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi badala ya kukaa vijiweni.
PIX 3
Afisa Vijana wa Halmashauri ya Nzega Bi.Frida Lwani (watatu  kulia) akifafanua jambo kuhusu maendeleo ya vikundi vya vijana vya  hapo kwa Maafisa kutoka Wizara ya habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo walipowatembelea katika ofisi ya halmashauri ya Nzega hivi karibuni.
“Serikali imedhamiria kwa dhati kuwakomboa vijana kiuchumi kwa kutambua changamoto ya ajira iliyopo katika taifa letu  kwa sasa na dunia nzima kwa ujumla”,alisema Bw.Mtawa.
Pamoja na hayo naye Mwenyekiti wa Vijana Saccoss Nzega Bw.Emmanuel Mambo, ameishukuru serikali kwa niaba ya vijana wa Nzega kupitia Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kuwapatia fedha hizo walizoomba kwa ajili ya kufanya miradi mbalimbali ikiwemo ufugaji na kilimo itakayoongeza kipato chao.
 

MTUKURU waua mtoto wa mwaka mmoja Singida

DSC03164
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida, ACP Thobias Sedoyeka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake.
Na Nathaniel Limu, Singida
POLISI mkoani Singida inamshikilia mwanamke mmoja kwa tuhuma ya kusababisha kifo cha mtoto wa mwaka mmoja na mama mtoto kulazwa baada ya kunywa pombe ya ‘Mtukuru’ nyumbani kwa  mtuhumiwa.
Kamanda wa polisi mkoa, Thobias Sedoyeka alimtaja mwanamke anayeshikiliwa kuwa ni Anastazia Kadama (35) mkazi wa kijiji cha Msule, Misughaa wilayani Ikungi mkoani Singida.
Alisema kuwa tukio hilo ni la Jan 07 mwaka huu majira ya saa 3.15 asubuhi kijijini hapo.
Alisema kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa Anastazia aliandaa pombe ya kienyeji iitwayo ‘Mtukuru’ kwa ajili ya kuwaalika majirani kwenda kumsaidia kulima shamba lake lakini kwa bahati mbaya siku hiyo mvua kubwa ilinyesha kiasi cha kuzuia shughuli hiyo kufanyika.
Kutokana na kuhofu pombe hiyo kuharibika, mtuhumiwa inadaiwa kuwa aliamua kuigawa kwa watu ili wainywe bure; mmoja wa watu hao akiwa mama wa mtoto aliyekufa, Magdalena Muna.
Alisema kuwa baada ya Magdalena kuionja pombe hiyo alimpa mtoto wake wa mwaka mmoja, Josephat Ntui, naye akanywa.
Kamanda Kamwela alisema kuwa baada ya Magdalena na mtoto wake kunywa pombe hiyo, walianza kutapika na kuharisha jambo lililosababisha wakimbizwe hospitali ya misheni Makiungu kwa ajili ya matibabu.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa mtoto huyo alizidiwa njiani kisha akafariki dunia kabla ya kufikishwa hospitalini lakini mama yake alifika akiwa hai na bado anaendelea na matibabu.
Kufuatia tukio hilo, Kamanda Kamwela amewataka wakazi wa mkoa huu kuwashirikisha wataalamu wa afya katika shughuli zao mbalimbali  za kuchinja, kuandaa chakula au pombe za kienyeji ili kuepukana na matatizo yasiyo ya lazima.

TRA MKOA WA SINGIDA, YATOA MSAADA WA MADAWATI WILAYA YA MKALAMA

DSC03256
Meneja TRA mkoa wa Singida, Samson Jumbe (kushoto) akimkabidhi Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Isanzu wilaya ya Mkalama, Sadick Mbiro Abdallah, msaada wa madawati 25 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili. Katikati mwenye miwani ni Afisa elimu kwa umma (TRA),Zakaria.
(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Mkalama
Meneja wa mamlaka ya mapato (TRA) Tanzania mkoani Singida, Samsoni Jumbe,amewahimiza  viongozi/watendaji na watu wenye uwezo kiuchumi kujenga utamaduni  wa kushiriki ukarabati  majengo na miundombinu mingine ya shule/vyuo walikosomea, ili iendelee kuvutia kama ilivyokuwa wakati wa enzi zao.
Jumbe ametoa wito wakati akizungumza na uongozi wa shule ya msingi ya Isanzu Wilaya ya Mkalama, muda mfupi kabla hajakabidhi  madawati 25 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili.
Alisema uzoefu unaonyesha shule nyingi  pamoja na vyuo mbalimbali vilizojengwa miaka  mingi, vingi zimechakaa vibaya na majengo yake mengi hayafai kutumiwa na wanafunzi  na walimu.
Aidha, Jumbe alisema kuwa majengo na miundombinu mingine ya aina hiyo inafika mahali haivutii tena na yanakuwa ni hatari kwa usalama wa wanafunzi na walimu hao.
DSC03252
Meneja wa mamlaka ya mapato (TRA) mkoa wa Singida, Samson Jumbe akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Isanzu iliyojengwa na Wajerumani mwaka 1934.Wanafunzi hao wamekalia madawati 25 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili yaliyotolewa msaada na TRA mkoa wa Singida.
“Shule za Msingi walikopita viongozi wa ngazi  mbalimbali wakiwemo wa kitaifa na wabunge,  na wafanya biashara  wa ngazi mbalimbali, zimejengwa miaka mingi kama hii ya Isanzu iliyojengwa na Wajerumani mwaka 1934. Ni lazima zichakae kwa hiyo zinahitaji ukarabati  mkubwa ambao gharama zake kwa kawaida ni kubwa”,alifafanua meneja huyo.
Jumbe alisema viongozi waliosomea katika shule/vyuo hivyo hawana budi kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule /vyuo kutafuta fedha ikiwemo kwa kuandaa harambee kwa lengo la kupata fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo na miundombinu mingine na ununuzi wa madawati.
Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo Sadick Mbiro Abdallah, alisema shule hiyo yenye wanafunzi zaidi ya  600, inahitaji madawati 204 yaliyopo ni 110 mapungufu ni dawati 94.
DSC03262
Moja ya madarasa yaliyojengwa mwaka 1934 na Wajerumani ya shule ya msingi Isanzu wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida.Viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida na aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki Mgana Msindai na David Holela aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Ushirika wamesoma katika shule hiyo.Kwa sasa darasa hilo bado linaendelea kutumika.
Katika hatua nyingine mwalimu Abdallah alisema shule hiyo ambayo imetoa wasomi wengi wakiwa ni akina Mgana Msindai  Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Singida na  David Holela aliyewahi kuwa Naibu waziri wa ushirika, inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mwamko duni wa elimu kwa  wazazi/walezi wengi wa wanafunzi wa shule hiyo.
Akifafanua, alisema wazazi/walezi wengi wa wanafunnzi wa shule hiyo wamekuwa wakiwatisha watoto wao na kuwaagiza wahakikishe hawafaulu hasa mtihani wa Taifa wa Kumaliza elimu ya Msingi.
“Mwanafunzi anaweza kuwa na uwezo mzuri darasani kuanzia darasa la kwanza hadi la saba. Lakini utashangaa matokeo  ya mtihani wa Taifa na darasa wa darasa la saba   kwani, atafanya vibaya mno”,alifafanua.na kuongeza; “Hali hii inachangiwa na wazazi/walezi kuwaonya watoto wao kwamba wakifaulu kwenda sekondari watajisomesha wao wenyewe.
Kwa mujibu wa Mwalimu Abdallah mwaka juzi wanafunzi 15 kati ya 66 walifaulu mtihani wa Taifa wa kumaliza elimu ya msingi mwaka jana wanafunzi 10 kati ya 66 walifaulu mtihani wa Taifa wa Darasa la saba.

NAIBU WAZIRI WA MAJI AZINDUA MIRADI YA MAJI MIWILI KATIKA WILAYA YA MBEYA VIJIJINI.

NA 







Naibu waziri wa maji na Mbunge wa jimbo la mvomero Mh, Amos Makala amezindua miradi ya maji miwili ilioko katika wilaya ya Mbeya, mmoja umejengwa katika kata ya tembela kijiji cha galijembe na mmoja umejengwa katika kata ya Igale na Shongo.

Aidha Makala ameahidi kupeleka shilingi milioni mia moja tisini na tano katika kata ya Iwindi wilaya ya Mbeya vijijini ikiwa fedha hizo anatarajia kutok  serikalini.

Friday, 9 January 2015

Stars maboresho kuivaa Rwanda

Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kitacheza mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya Rwanda itakayofanyika Januari 22 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mechi hiyo ni sehemu ya programu ya Kocha Mart Nooij kuiandaa timu hiyo kwa ajili ya mechi za mchujo michuano ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN).
Mechi za mchujo za michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Rwanda zinaanza Mei mwaka huu.
Kocha Nooij anatarajia wakati wowote kutangaza kikosi cha timu hiyo inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kitakusanyika Januari 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam, na siku moja baadaye kwenda jijini Mwanza.

Bangi yamtia jela mwanawe Jackie Chan

Jackie chan na mwanawe Jacee Chan
Jacee Chan mwana wa mwana nyota wa filamu Jackie Chan amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela kwa kutumia mihadarati.
Chana mwenye umri wa miaka 32 alikiri kufanya makosa hayo katika mahakama ya wiliaya ya mjini Beijing Dongcheng kwa kuwaficha wengine ili kutumia dawa za kulevya.
Polisi walivamisa nyumba yake mnamo mwezi Agosti na kupata gramu 100 za marijuana.
Alikabiliwa na hukumu ya miaka mitatu.
Kukamatwa kwake kunajiri kufuatia msako wa dawa za kulevya nchini Uchina ambapo watu kadhaa mashuhuri walikamatwa.
Jacee Chan na babaake jackie Chan
Mnamo mwezi Juni mwaka 2014,rais Xi Jinping aliwaagiza polisi kutumia mikakati mikali ili kusitisha utumizi wa mihadarati.
Kukiri kwa mwana wa mcheza filamu mashuhuri nchini Uchina kunatoa ujumbe muhimu kutoka kwa serikali ya Uchina.
Hakuna aliye na kinga nchini Uchina katika msako huo wa dawa za kulevya.
Chan na nyota wa filamu kutoka Taiwan Kai Ko mwenye umri wa miaka 23 walikamatwa pamoja katika nyumba ya Beijing mnamo mwezi Agosti huku polisi wakisema kuwa walipatikana wametumia bangi.

Washukiwa wa mauaji Ufaransa wauawa

Vyombo vya habari nchini Ufaransa vimeripoti kwamba washukiwa wawili waliohusika na mauaji ya Charlie Hebdo wameuawa.
Wawili hao walisakwa kwa siku mbili na polisi baada ya kutoroka baada ya kuwaua wandishi habari wa jarida la Charlie Heblo.
Maafisa wa usalama walivamia eneo ambako vijana hao walikuwa wamejificha wakiwa na mateka mmoja na kuwaua vijana hao ambao walikuwa ndugu.
Milio ya risasi ilisikika huku moshi mkubwa ukionekana kufuka kutoka katika jengo hilo huku makomando wakionekana wakivamia jengo hilo.
Duru zinasema washukiwa hao walikuwa wamejihami walifyatulia risasi makomando hao kabla ya kuuawa.
Walisema waliwaua wandishi wa habari kama hatia ya kulipiza kisasi hatua ya wahariri wa jarida hilo kuchora vibonzo kumkejeli mtume Mohammed wa dini ya kiisilamu.
Iliarifiwa walikipora kituo cha mafuta wakiwa mbioni huku wakiwateka mateka na kwenda nao katika kiwanda ambako walikuwa wamejificha.
Mateka mmoja aliweza kuokolewa.
Kwingineko milipuko na milio ya risasi ilisikika ndani ya duka la jumla la kiyahudi, Kaskazini mwa mji huku watu watano waliokuwa wametekwa nyara na mshambuliaji mmoja wakiuawa.
Baada ya operesheni ya polisi kukamilika baadhi ya matyeka wlaiokuwa wamezuiliwa ndani ya duka hilo walionekena wakitoka nje.

WillY m -- Hope u need me( official video)

Monday, 29 December 2014

Timu ya taifa ya Tanzania yaanza kambi leo Dar es Salaam




Timu ya taifa ya Tanzania inaanza kambi leo Dar es Salaam kujiandaa na michuano ya kriketi ya Afrika chini ya miaka 19 daraja la 1 itakayofanyika nchini Namibia mapema mwakani.
Kambi hiyo chini ya kocha mchezaji Hamis Abdallah inakuja baada ya majuma mawili ya michuano ya majaribio yaliyofanyika Nairobi, Kenya huku Tanzania ikishika nafasi ya tatu baada ya wenyeji kuwafunga Uganda.
Namibia itakuwa wenyeji wa michuano hiyo itakayokuwa ni sehemu ya kufuzu kucheza kombe la dunia chini ya miaka 19.
A wali michuano hiyo ilipangwa kuanza Januari Mosi na kupelekwa mbele hadi Februari.
Kenya na Uganda zitakuwa miongoni mwa nchi shiriki kutoka Afrika Mashariki na michuano ya Nairobi ilikuwa na lengo la kuziandaa timu zao.
Abdallah ameiambia BBC kuwa baada ya mapumziko ya Christmas wanaanza mazoezi wakiwa na ari na nguvu.
Timu ya Tanzania hivi karibuni ilichukua ubingwa Wa Afrika chini ya miaka 19 ligi daraja la 2, hivyo kufuzu michuano ya Namibia itakayoanza mapema mwezi wa pili

Mashindano ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake kuzinduliwa Januari Mosi


Mashindano ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Taifa Cup Wanawake) yanazinduliwa rasmi Januari Mosi mwakani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwa mechi kati ya wenyeji Mwanza na Mara. Mechi hiyo itakayoonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam itachezwa kuanzia saa 10 jioni. Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Proin yatachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini katika hatua ya kwanza.
Januari 10 mwakani ndipo zitachezwa mechi kwa mikoa yote ambapo Geita itakuwa mwenyeji wa Kagera (Uwanja wa Geita), Tabora vs Kigoma (Ali Hassan Mwinyi), Simiyu vs Shinyanga (Uwanja wa Simiyu), Arusha vs Manyara (Sheikh Kaluta Amri Abeid), na Kilimanjaro vs Tanga (Uwanja wa Ushirika).
Mechi nyingine ni Lindi itaikaribisha Mtwara kwenye Uwanja wa Ilulu, Ruvuma vs Njombe (Uwanja wa Majimaji), Mbeya vs Iringa (Uwanja wa Sokoine), Katavi vs Rukwa (Uwanja wa Katavi), Dodoma vs Singida (Uwanja wa Jamhuri) na Pwani itakuwa mwenyeji wa Morogoro katika Uwanja wa Mabatini.
Timu hizo zitarudiana Januari 13 mwakani, ambapo baada ya matokeo ya nyumbani na ugenini timu iliyoshinda ndiyo itakayoingia hatua inayofuata ambayo pia itashirikisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke.
Hatua hiyo, mechi zake za kwanza zitachezwa Januari 17 mwakani wakati zile za marudiano zitafanyika Januari 21 mwakani.
Baada ya hapo, hatua itakayofuata ni robo fainali, nusu fainali na fainali ambayo ndiyo itakayotoa bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini.
Mdhamini atatoa jezi kwa timu zote zinazoshiriki kabla ya kuanza mashindano hayo.

ndege ya AirAsia ambayo ilipotea jana Jumapili imeendelea leo tena baada ya kusitishwa kwa muda.

Shughuli ya kutafuta ndege ya AirAsia ambayo ilipotea jana Jumapili imeendelea leo tena baada ya kusitishwa kwa muda.
Watu 162 walikuwa kwenye ndege hiyo wakati ikipoteza mawasiliano na kituo cha kuelekeza safari za ndege. Ndege hiyo ilikuwa safarini kwenda nchini Singapore ikitokea mji wa Surubaya nchini Indonesia. Shughuli za kuitafua zinafanyika kwenye kisiwa cha Belitung.
Ndege za kijeshi kutoka indonesia na singapore zilikuwa zikiisaka ndege hiyo kusini magharibi mwa pwani ya Borneo ambapo ndege hiyo ilitoweka.

Abiria miamoja wakwama:ATC

  

Shirika la ndege Tanzania ATC
Zaidi ya abiria mia moja wa ndege ya ATC wamekwama nchini Tanzania, baada ya safari zao kuarishwa. Wengi wao wakielekea nchini Comoros na wengine wakiwa katika safari za ndani, kuelekea Mtwara na Kigoma wamekwama kwa siku mbili mjini Dar es salaam.
Abiria hao imebidi wakodiwe hoteli ilivyo ada wakisubiri muafaka wa namna watakavyosafiri kuelekea Comoro. Sharifu Hashim, Balozi wa heshima wa Comoro huko Chicago nchini Marekani, anasema mambo yake mengi yamekwama kutokana na tukio hili na hajapata uhakika ataondoka lini
Zenabal Mwarabu yeye hofu yake ni kwa namna gani ataweza kuiwahi ndege aliyokuwa aunganishe Kisiwani Comoro kuelekea katika kisiwa kingine cha Rarinyo.
Msawi Seifu anasema ijapokuwa tatizo hili limetokea lakini Air Tanzania ni mkombozi kwa wana Comoro….Lily Fungamtama, Mkuu wa Kitengo cha Biashara amesema tayari Air Tanzania inashughulika kuhakikisha abiria wote wanasafiri mapema kesho .
Sikukuu za mwisho wa mwaka ndilo tatizo la kukwama kwa abiria hao,kwani marubani hawajarejea kazini tangu walipoondoka, na walitegemewa kurejea kazini tarehe 27 mwezi huu, baada ya sherehe za Christimas, lakini haikuwa hivyo na kusababisha sintofahamu hiyo.

Wednesday, 24 December 2014

Bolton yamsajili mgongwe E mile heskey kwa mkataba wa muda mfupi

 

Klabu ya Bolton Wanderers imetangaza kumsajili mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Uingereza Emile Heskey kwa mkataba wa muda mfupi.
Heskey mwenye umri wa miaka 36 amekuwa akifanya mazoezi na klabu hiyo huku akikitumikia kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 21 katika mchezo dhidi ya Reading Jumatatu iliyopita.
Mkongwe huyo ambaye ameitumikia Uingereza mechi 62 alikuwa akicheza katika klabu ya Newcastle Jets ya Australia ambayo ilimuachia April mwaka huu.
Bolton kwasasa inasubiri ITC ya mshambuliaji ili kukamilisha usajili wake.

Huyu ndiyo ww jamaa aliye kula tumbo mayai 150 na mayai ya kuku 10 kwa dakika 37

A man challenged himself to eat 150 quail eggs and 10 chicken eggs in 37 minutes at a restaurant in Changsha, central China's Hunan province, December 23. ,   yu

Amwacha mumewe na dadake uchi baada ya wakifanya mapenzi

 

Wawachwa uchi

Mwanamke kwa jina Ting Su nchini Uchina alimwacha mumewe na dadake bila nguo barabarani baada ya kuwapata wakifanya mapenzi Ting Ting Su aligundua kwamba mumewe alikuwa akimdanganya na dadaake na kuwafuata hadi katika kituo kimocha cha maduka akitumia teknologia katika simu yake ambapo aliwapata wakichemshana katika gari la mumewe.
Wawili hao walitoka ndani ya gari hilo bila nguo kwa kubabaika ili kujaribu kumuelezea kilichokuwa kikendelea lakini waliwachwa na mshangao mkubwa wakati Ting alipoingia ndani ya gari hilo na kuondoka kwa haraka na kuwawacha wawili hao barabarani bila nguo.
Kulingana na gazeti la Metro,shahidi aliyejulikana kama You Meng alisema walioshuhudia kisa hicho walibeba simu zao na kuanza kuchukua picha na yeye hakubakia nyuma.
Mumuwe aligonga dirisha la gari hilo na kumpigia kele mkewe lakini hakujali kamwe aliliondosha gari hilo kwa haraka.

APORWA NA KUJERUHIWA KWA RISASI

Mpita njia ajeruhiwa kwa Risasi na Majambazi waliovamia na kupora ktk duka la Pesa Morocco Kinondoni


Less than one hour ago here at Morocco nyuma ya Airtel Building a lady was shot to dead!!

Bodaboda walivamia kiduka cha M-PESA, tiGO PESA na Airtel Money; wakati wanaondoka wakawa wanapiga risasi ikampata huyu dada alikuwa anajipitia barabarani hajui hili wala lile.


- Kumbe huyu dada hakufa. Risasi ilimpalaza upande wa kulia. Walimshoot baada ya kuonekana anaongea na simu, baada ya tukio la kumuibia dada mwingine, ambaye inasemekana alikuwa ametokea Mlimani City na Hela.

- Taarifa za usiku wa leo, Disemba 23, 2014 zinadai Glory kaaga dunia! R I P
 

Wednesday, 17 December 2014

MUNGU WANGU MSAIDIZI WA MAXIMO NAYE ASEPA KWENDA KWAO BRAZIL


NEIVA...


Kocha Msaidizi wa Yanga, Leonardo Neiva naye yuko njia moja kurejea kwao.
Taarifa za uhakika zinaeleza, Neiva anaondoka na nafasi yake itachukuliwa na Boniface Mkwasa.

Usiku wa kuamkia jana kumekuwa na kikao kizito cha viongozi wa Yanga kujadili mustakabari wa Wabrazil hao.
"Ni kweli Neiva ataondoka, hilo suala limejadiliwa. Maana anatakiwa Mkwasa kuja kuziba nafasi yake," kilieleza chanzo.

"Kama akija kocha Pluijm, lazima atataka kufanya kazi na Mkwasa."



Tuesday, 16 December 2014

VAN GAAL KOCHA BORA WA MWAKA, VAN PERSIE ABEBA TUZO, ROBBEN MWANA MICHEZO BORA


kocha louis van gaal ameibuka na kupewa tuzo ya kocha bora wa mwaka wa uholanzi baada ya kuifikisha nchi hiyo kwenye nusu fainali ya kombe la dunia 2014. mshambuliaji wake, robben van persie amepewa tuzo ya bao bora, lile alilofunga kwenye kombe la dunia akipaa kama ndege na mshambuliaji wa bayern munich, arjen robben ameteuliwa kuwa mwanamichezo bora wa mwaka wa uholanzi. tuzo hizo zimefanyika juzi usiku nchini humo.





Amissi Tambwe kutua Yanga asema Ndipo alipo pataka ili awaanyeshe makali walio muacha

  
tambwe yanga
 HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa dakika chache zilizopita ni kwamba klabu ya Yanga imemsajili mshambuliaji wa Simba aliyeachwa Amisi Tambwe .
 Yanga imemsajili Tambwe dakika chache zilizopita ambapo anakuja kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Emerson Oliveira wa Brazil aliyetemwa kwa kukosa ITC.
Tambwe ametua Yanga ikiwa ni siku chache baada ya Mganda Hamis Kiiza kuachwa na klabu hiyo na kukimbilia URA ya Uganda baada ya Kpeh Seen Sherman wa Liberia kupewa kandarasi ya kuichezea timu hiyo.
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
 Tambwe alikuwa mfungaji bora wa ligi msimu uliopita ambapo alifunga mabao 19 kwenye ligi lakini alishindwa kuwika msimu huu baada ya kutopewa nafasi ya kutosha chini ya Patrick Phiri.
 Simba imemuacha Tambwe baada ya kumsajili Danny Serunkuma toka Gor Mahia ya nchini Kenya .
 Yanga imekamilisha usajili huu saa chache kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa leo na TFF.

Sakata la Escrow lafanya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema kuaachia ngazi



http://2.bp.blogspot.com/-HfIVzV9HEPE/Uq2Qh28re9I/AAAAAAAALfk/iZ76iAX0yLA/s640/1.png
jaji Werema aliyetangaza kuachia ngazi mwenyewe

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ametangaza kujiuzulu nafasi yake hiyo.
Habari hizo zinasema Jaji Werema mmoja wa vigogo wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la uchotwaji wa fedha za Akaunti za Tegeta Escrow zipatazo zaidi ya Sh Mil 300.
Kwa mujibu wa taarifa hizo zinasema kuwa Jaji Werema ameamua kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake na kwamba Rais Jakaya Kikwete ameafikiana na maamuzi hayo na kumshukuru kwa ujtendaji wake na kumtakia kila la heri katika maisha yake mapya.
Hata hivyo taarifa hizo zinasema kuwa, maamuzi hayo yamekuja baada ya shinikizo kubwa ambalo limekuwa likitolewa kila pembe ya nchi kwa Rais JK kuwawajibisha wote waliotajwa kwenye mapendekezo nane ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuhusiana na sakata hilo ambalo limeitia doa Tanzania mbele ya nchi wahisani.

Monday, 15 December 2014

Breaking news ya kocha Marcio Maximo kuondoka Yanga.


BreakingHabari rasmi toka ndani ya klabu ya Yanga zinasema kuwa kocha Mbrazil Marcio Maximo ameondoka ndani ya klabu hiyo ambapo habari hizi zinakuja dakika chache baada ya vyombo vya habari kuripoti tetesi zinazohusu mustakabali wa kocha huyo Mbrazil.
Maximo anaondoka Yanga baada ya uongozi wa klabu hiyo kukubaliana naye kuvunja mkataba aada ya kushindwa kuelewana juu ya jinsi ya kuiendesha klabu hiyo kwenye masuala ya ufundi.
Yanga ilishikilia msimamo wa kumuajiri Mkurugenzi wa ufundi ambaye alipangwa kuwa Charles Boniface Mkwasa jambo ambalo Maximo hakukubaliana nalo.
Nafasi ya Maximo sasa itachukuliwa na Mholanzi Hans Van Der Pluijm ambaye aliifundisha timu hiyo kwa nusu msimu baada ya kufukuzwa kwa Mholanzi mwenzie Ernst Brandts.
Tukio hili linaendeleza historia ya Yanga kufukuza makocha baada ya kufungwa na Simba kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe baada ya kufukuzwa kwa Ernst Brandts msimu uliopita kufuatia kipigo cha 3-1 mbele ya Simba iliyokuwa inaongozwa na Dravko logarusic.

Simba kusajili beki, kutoka mtibwa sukari usiku wa leo kabla ya kufungwa kwa usajili


Katika usiku ambao umekuwa na movement nyingi za wachezaji na makocha , klabu ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa pembeni toka timu ya Mtibwa Sugar, Hassan Kessy.
Beki huyo ambaye ametokea kuwa mmoja kati ya wachezaji wa kutumainiwa kwenye klabu hiyo ya wakata miwa wa huko Manungu Turiani mkoani Morogoro, anaungana na wachezaji wapya waliosajiliwa katika kipindi hiki cha dirisha dogo ambao ni Simon Sserunkuma, Danny Sserunkuma, na Juko Murshid wote kutoka Uganda.
Kessy ambaye ametajwa kuwa moja kati ya wachezaji wanaokaribia kuwa mmoja ya wachezaji wa Timu ya Taifa Stars alichezea Mtibwa kwa mara ya mwisho katika mchezo wa kirafiki ambao ilifungwa na Azam Fc 3-1.
hassan kessy
Beki huyu anasajiliwa baada ya mazungumzo ya muda mrefu yaliyofanyika chini ya usimamizi wa viongozi wa Simba wakiongozwa na Geoffrey Nyange Kaburu na Kiongozi wa Mtibwa, Jamal Bayser.
Tetesi zaidi zinasema kuwa Simba imemsajili beki huyo kwa thamani ya shilingi milioni 30.