Na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Mwanza.
SERIKALI
imetoa ufafanuzi wa bei za Mashine za Kodi za Kielektroniki (EFDs) kwa
wafanyabiashara kurahisisha ulipaji wa kodi na kufanya biashara yenye tija na ubora nchini.
Kauli
hiyo ilitolewa na Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato nchini
Patrick Kasera alipokuwa akifafanua na kutoa maelekezo ya bei ya
mashine hizo kwa nyakati tofauti jijini Mwanza na Musoma akiwa miongoni
mwa wajumbe wa msafara wa Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima katika mikoa
ya kanda ya Ziwa.
Kamishna
Kasera alisema kuwa bei ya chini ya sasa ya mashine za EFD ni
sh.600,000/= za kitanzania na gharama ya juu ni sh. 690,000/=.ambapo bei
hizo zote zinajumuisha gharama usafirishaji.
Bei
iliyotolewa na serikali ni tofauti naile ambayo ilikuwa inawapotosha
wafanyabiashara mitaani kuwa ni sh. 80,000/= ambayo si sahihi kulingana
na bei halali iliyotolewa na serikali.
“Serikali
haifanyi biashara ya kuwaumiza, kuwanyanyasa na kuwaonea na hakuna
faida yeyote inayopata inapofanya hivyo kwa watu wake” alisema Kasera.
Kamishna
Kasera alisema kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki
yanayorahisisha walipa kodi iliwaweze kutunza kumbukumbu za biashara zao
kwa usahihi na usalama kwa kutumia kifaa maalumu kinachoitwa “Fiscal
Memory” badala ya mfumo wa zamani wa kuandika kwa mkono.
Mashine
hizi ni msaada na zina faida kubwa kwa wafanyabiashara wenyewe ambapo
zitaasaidia kutunza kumbukumbu zaidi ya miaka mitano kama sheria
inavyotaka.
Kwa
upande wa serikali, mashine hizi zitasaidia kutumia kodi zilizokusanywa
kutoa mahitaji ya kijamii na kiuchumi kwa wakati kwa wananchi wake
ambapo itakuwa nia rahisi kupanga uchumi na kukadiria mapato yake kwa
wakati na kwa usahihi.
Kamishna
Kasera ametoa rai kwa mwananchi yeyote atakayetaja majina ya watu
wanaokwepa kulipa kodi kwa manufaa yao wenyewe na umma kwa ujumla ofisi
yake itatoa tuzo kwa atakayefanya hivyo.
“Waleteni watu wanaokwepa kulipa kodi ili mtajirike” alisisitiza Kamishna Kasera.
Rai
hiyo kwa mujibu wa Kamishna Kasera iliyoitoa nafasi kwa mtu yeyote
kutoa taarifa kwa vyombo husika na kwamba mtoa taarifa atazawadiwa
kitita cha hadi sh. Milioni 20 za kitanzania na jina la mtoa taarifa
litahifadhiwa.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara mkoa wa Mara
Baltazari Mwita kwa niaba ya wafanyabiashara alimshukuru Mgeni rasmi
Naibu Waziri wa Fedha Adam Mlima na ujumbe wake kuwa tayari kukaa na
wafanyabishara kwa takribani zaidi ya masaa manne kuwaelimisha juu ya
matumizi sahihi ya mashine za EFD na faida zake.
Mwenyekiti
huyo amemwahidi Naibu Waziri Malima kuwa wafanyabiashara wote wapo
tayari kufuata elimu waliyopewa katika mkutano huo kwa manufaa yao
wenyewe na taifa kwa ujumla.
Naye
mfanyabiashara wa jijini Mwanza Leopord Kurugira alisema kuwa
wafanyabiashara hawana shida na mashine za EFD, wao wanahitaji kupewa
elimu zaidi juu ya mashine hizo.
Zaidi
ya hayo Karugura alimshukuru Naibu Waziri na ujumbe wake kuongea nao na
kuwapa elimu ya mashine za EFD ambazo mwanzoni wao kama wafanyabiashara
hawakupata elimu ya kutosha na kuwasababisha kuziogopa badala ya
kuzitumia.
Kamishna
Kasera aliifafanua zaidi kwa wafanyabiashara wa mkoani Mara na Mwanza
juu ya mashine za EFDs na alisema kuwa mashine hizo kazi yake kuu ni
kutunza kumbukumbu za biashara hasa manunuzi na uuzaji wa bidhaa na
huduma mbalimbali na sio mfumo wa kodi kama ilivyopokelewa mwanzoni na
wafanyabiashara nchini.
Mashine
za EFD ambazozinatumika zipo za aina tatu ambazo ni Rejesta za kodi za
Kielektroniki (ETR), Printa za Kielektrniki za kodi (EFP) na Mashine za
Alama za Kielektroniki za kodi.
Ziara
ya Naibu Waziri wa Fedha ililenga kutembelea vituo vya forodha, TRA vya
Rusumo, Kyaka, Mtukula na Bukoba mjini katika mkoa wa Kagera, Tarime,
Sirari na Musoma mjini katika mkoa wa Mara na jijini Mwanza ambapo pote
alipotembelea alizungumza na wafanyabiashara katika mikoa hiyo ya Kanda
ya Ziwa.













0 comments:
Post a Comment