MABINGWA
wa Tanzania Bara, Yanga, wanatarajiwa Alhamisi hii kuondoka Nchini
kuelekea Uturuki kwa Kambi ya Mazoezi ya Wiki mbili huku wakiwa na
Kikosi chao chote.
Hii itakuwa mara ya pili kwa Yanga
kwenda Uturuki kufuatia Ziara kama hii Mwezi Desemba Mwaka 2012
walipopiga Kambi Mji wa Antalya ulio Kusini Magharibi mwa Uturuki.

Walipokuwa huko, kwenye Ziara
iliyomalizika Januari Mwaka Jana, Yanga walicheza Mechi kadhaa za
Kirafiki dhidi ya Timu kubwa za Nchi hiyo na kutia fora kwa Kandanda
lao.
Kwenye Ziara hii huenda Yanga isimchukue
Kiungo wao Athumani Idd ‘Chuji’ ambae inadaiwa anakabiliwa na tuhuma za
utovu wa nidhamu kwenye pambano la Nani Mtani Jembe ambalo Yanga
ilifungwa 3-1 na Simba.
Inadaiwa kwenye Mechi hiyo Chuji
alipobadilishwa katika Kipindi cha Pili hakukaa Benchi na moja kwa moja
alielekea Vyumba vya Kubadili jezi na kisha kutokomea nje ya Uwanja.
Kwa vile Yanga wapo kwenye mchakato wa
kusaka Kocha Mkuu baada ya kumwondoa Ernie Brandts kutoka Uholanzi,
Ziara hii ya Yanga huko Uturuki itakuwa chini ya Kocha Msaidizi Charles
Boniface Mkwasa na Kocha wa Makipa, Juma Pondamali ni mahsusi kwa ajili
ya Raundi ya Pili ya Ligi Kuu Vodacom inayoanza Januari 25, Mashindano
ya CAF CHAMPIONZ LIGI, ambayo Yanga itacheza na Klabu ya Comoro,
Komorozine, Mwezi ujao na pia Kagame Cup, Kombe la Klabu Bingwa Afrika
ya Mashariki na Kati.
LIGI KUU VODACOM
MSIMAMO:
|
NO
|
TEAMS
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
|
1
|
Young Africans |
13
|
8
|
4
|
1
|
31
|
11
|
20
|
28
|
|
2
|
Azam FC |
13
|
7
|
6
|
0
|
23
|
10
|
13
|
27
|
|
3
|
Mbeya City |
13
|
7
|
6
|
0
|
20
|
11
|
9
|
27
|
|
4
|
Simba SC |
13
|
6
|
6
|
1
|
26
|
13
|
13
|
24
|
|
5
|
Kagera Sugar |
13
|
5
|
5
|
3
|
15
|
10
|
3
|
20
|
|
6
|
Mtibwa Sugar |
13
|
5
|
5
|
3
|
19
|
17
|
2
|
20
|
|
7
|
Ruvu Shootings |
13
|
4
|
5
|
4
|
15
|
15
|
0
|
17
|
|
8
|
Coastal Union |
13
|
3
|
7
|
3
|
10
|
7
|
3
|
16
|
|
9
|
JKT Ruvu |
13
|
5
|
0
|
8
|
10
|
16
|
-6
|
15
|
|
10
|
Rhino Rangers |
12
|
2
|
4
|
6
|
9
|
16
|
-7
|
10
|
|
11
|
JKT Oljoro |
13
|
2
|
4
|
7
|
9
|
19
|
-10
|
10
|
|
12
|
Ashanti United |
13
|
2
|
4
|
7
|
12
|
24
|
-12
|
10
|
|
13
|
Tanzania Prisons |
12
|
1
|
5
|
6
|
6
|
16
|
-10
|
8
|
|
14
|
Mgambo JKT |
13
|
1
|
3
|
9
|
3
|
23
|
-20
|
6
|
RATIBA
RAUNDI YA PILI
25 Januari 2014
Ashanti United v Yanga
Azam FC v Mtibwa Sugar
Coastal Union v JKT Oljoro
Kagera Sugar v Mbeya City
Tanzania Prisons v Ruvu Shootings
JKT Ruvu v Mgambo JKT
Simba v Rhino Rangers












0 comments:
Post a Comment