Monday, 20 January 2014

VERGINI ATUA SUNDERLAND, TRAORE AKARIBIA EVERTON, ANELKA AZUA BALAA WBA!!

>>“QUENELLE" YA NICOLAS ANELKA YAWATOA MKUKU ZOOPLA WBA!!
ANELKA-SALUTEVIKUMBO vya Uhamisho wakati huu wa Dirisha la Uhamisho la Mwezi Januari vimeshamiri huku huko West Bromwish Straika wa France, Nicolas Anelka, akizua balaa kubwa.
SOMA ZAIDI:
LACINA TRAORE: EVERTON WAKARIBIA KUMSAINI MKOPO TOKA MONACO
Straika wa Monaco Lacina Traore anatarajiwa kupimwa Afya yake Klabuni Everton ili kumalisha Uhamisho wake wa Mkopo.
Awali iliaminika Straika huyo kutoka Ivory Coast mwenye Miaka 23 na Urefu wa Futi 6 Inchi 8 anakwenda West Ham baada Klabu hiyo ya London kumwombea Kibali cha Kazi cha Nchini Uingereza lakini Meneja wa West Ham, Sam Allardyce, ametoboa kuwa Straika huyo hataenda tena kwao.
Monaco wamemsaini Traore kutoka Anzhi Makhachkala ya Urusi ambako alicheza pamoja na Samuel Eto'o akitokea Kuban Krasnodar Juni 2012.
Kwenye Msimu wa 2012/13, Traore alifunga Bao 12 katika Mechi 24.
SUNDERLAND YAMSAINI KWA MKOPO SANTIAGO VERGINI
Sunderland imemsaini Beki wa Argentine Santiago Vergini kwa Mkopo hadi mwishoni mwa Msimu.
Vergini, Miaka 25, anatokea Klabu ya Uruguay Atletico Fenix ingawa alikuwa kwao Argentina akichezea Estudiantes kwa Mkopo.
Sentahafu huyo, ambae alianza kuichezea Timu ya Taifa ya Argentina Mwaka 2012, pia ameshaichezea Klabu ya Italy Verona na ile Klabu maarufu huko Argentina, Newell's Old Boys.
Vergini ni Mchezaji wa Pili kusainiwa na Sunderland Mwezi huu Januari na mwingine ni Beki kutoka Fiorentina ya Italy, Marcos Alonso, ambae pia yuko kwa Mkopo hadi mwishoni mwa Msimu.
QUENELLE" YA NICOLAS ANELKA YAWATOA MKUKU ZOOPLA WBA!!
Wadhamini wa West Brom, Zoopla, wameamua kuachana na Klabu hiyo mwishoni mwa Msimu kufuatia kitendo cha Nicolas Anelka kutumia Saluti iitwayo “Quenelle" ambayo inahusishwa na Mafashisti wa Nazi na Ubaguzi kwa Mayahudi.
Anelka, Miaka 34, alitoa Saluti hiyo ambayo Mkono mmoja unanyooshwa chini na mwingine kupita Kifuani na kuugusa mwingine, wakati alipofunga Bao kwenye Mechi na West Ham hapo Desemba 28.
Zoopla, ambae mmoja wa Wamiliki wake ni Myahudi Alex Chesterman, na ambao walikuwa wamalize Mkataba na WBA mwishoni mwa Msimu huu, Mkataba ambao ulianza 2012, wamesema watasaka Soko jingine.
Kitendo hicho cha Anelka bado kinachunguzwa na FA, Chama cha Soka England. Mwenyewe Anelka, mbali ya kuiahidi WBA kutoitumia tena, amekanusha Saluti hiyo kuhusishwa na Ufashisti na Ubaguzi na kubainisha inaitwa ‘Quenelle’ na ni kwa ajili ya kumsapoti Rafiki yake wa France, DieudonnĂ© M'Bala M'Bala, ambae ni Mchekeshaji, anaesakamwa Nchini humo kwa kudaiwa Mbaguzi.
Lakini Anelka si Mwanasoka wa kwanza kupigwa Picha akitoa hiyo ‘Quenelle’ kwani Samir Nasri wa Manchester City na Mamadou Sakho wa Liverpool walishanaswa wakiwa pamoja na DieudonnĂ© wakitoa Saluti hiyo  ingawa Sakho baadae alisisitiza hakujua maana yake na alihadaiwa kuitumia.

0 comments: