MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Sunday, 10 April 2016

Mwanamuziki Roma Mkatoliki Kafunga ndoa Jana Kwao Tanga.....

 PICHA 4: Roma Mkatoliki kafunga ndoa leo nyumbani kwao Tanga

on
Roma Mkatoliki ni msanii maarufu wa hiphop Tanzania ambaye kwenye upande wa pili wa maisha ameamua kufunga ndoa na mpenzi wake wa longtime ambaye wana mtoto pamoja (Ivan) na April 9 2016 ndoa imefungwa nyumbani Tanga na ni baada ya send-off kufanyika Dar es salaam February 2016.
roma 5
Roma 4
Roma 2
February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.
February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.
Roma Mkatoliki ni msanii maarufu wa hiphop Tanzania ambaye kwenye upande wa pili wa maisha ameamua kufunga ndoa na mpenzi wake wa longtime ambaye wana mtoto pamoja (Ivan) na April 9 2016 ndoa imefungwa nyumbani Tanga na ni baada ya send-off kufanyika Dar es salaam February 2016.

PICHA 4: Roma Mkatoliki kafunga ndoa leo nyumbani kwao TangaARE

Roma Mkatoliki ni msanii maarufu wa hiphop Tanzania ambaye kwenye upande wa pili wa maisha ameamua kufunga ndoa na mpenzi wake wa longtime ambaye wana mtoto pamoja (Ivan) na April 9 2016 ndoa imefungwa nyumbani Tanga na ni baada ya send-off kufanyika Dar es salaam February 2016.
roma 5
Roma 4
Roma 2
February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.
February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.

Hawa ndiyo wanawake Kumi Wanaofatiliwa na Kuandikwa Zaidi na Vyombo vya Habari


Inaweza ikawa mara ya kwanza kusikia neno”Socialite”,au pengine umeshawahi kusikia mtu akizielezea sifa za mtu kwa kumuita “Socialite person”,ila kwa kifupi “Socialite” ni neno la kingereza linalomwelezea mtu mwenye sifa nyingi ila baadhi ya sifa hizo ni pamoja na kuzungumziwa kwenye vyombo habari mara kwa mara,nguvu ya fedha,kuonekana kwenye matamasha na event mbalimbali za burudani,kujihusisha na masuala ya kijamii ect.Kwa kuzingatia sifa hizo hii hapa ni top ten socialite girls wanazungumziwa na kuandamwa zaidi na vyombo vya habari Afrika mashariki.

10:Hamissa Mobeto

Mrembo huyu ni mwanamitindo aliejipatia umaarufu kwa muda mfupi kwa kuonekana kwenye video kadhaa za mastaa wa bongo fleva kama “Your Mine” ya mwanamuziki Quick Racka na kupelekea watu wengi hasa magazeti ya udaku kumfatilia.


9:Gigy money 
Gigiy Money amejipatia umaarufu kwa miezi ya karibuni kwani licha kupiga picha zanazoonyesha maungo yake,ameonekana kwenye video nyingi za bongo fleva,baadhi ya video hizo ni “I get high” ya rapper Godzila, na”Shika adabu yako”ya Ney wa mitego,mbali kuonekana kwenye video hizo Gigy money ametajwa mara kadhaa kwenye headline za magazeti ya udaku akidaiwa kutoka kimapenzi na baadhi ya mastaa wa muziki.

8:Vanessa Chittle
Mrembo huyu ambae pia ana kipaji cha muziki,amekua akihost shows mbalimbali jijini Nairobi.Baada ya picha zake za utupu kuvuja kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya alipata umaarufu na kufanya watu wengi hasa magazeti yaudaku kuanza kumfatilia.

7:Risper Faith
Mrembo huyu mwenye shepu matata,amekua kwenye headline za magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii nchini Kenya kwa skendo za kutoka kimapenzi na watu maarufu,mbalina skendo hizo Risper amekua akidai kuwa yeye ni mkirsto na anaamini Yesu ameokoa maisha yake.


6:Judith Heard 
Mbali na kuonekana kwenye video ya Jose Chamilion inayofahamika kama “Vumilia”,mrembo huyu kutoka Uganda nimwanamitindo wa kimataifa na mjasiriamali ambae amekua kwenye headline za vyombo vya habari na mitandao ya kijamii nchini Uganda akidaiwa kutoka kimapenzi na vijana aliowazidi umri


5:Vera sidika 
Mrembo huyu alijipatia umaarufu mara baada ya kuonekana kwenye video inayofahamika kama”You Guy”ya kundi lamuziki la P-Unit iliyotoka mwaka 2012,mbali na video hiyo pia alionekana kwenye video inayofahamika kama “Carry Go” ya Nigerian musician Davido aliyomshirikisha D-Black,licha ya kutokeakwenye video hizo Queen V kama anavyojiita ameonekana kwenye season one ya reality show inayofahamika kama “Nairobi Diaries”.

4:Huddae Monroe
Mrembo huyu kutoka Kenya alijipatia umaarufu zaidi mwaka 2015 aliposhiriki kwenye shindano la “Big Brother Africa”,ingawa hakushinda ila Huddah ameendelea kubaki kwenye headline za media houses,magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii akiwa na skendo za kutoka kimapenzi na watu maarufu na mastaa wa muziki nchini Kenya.


3:Agness Masogange
Mrembo huyu mwenye shepu inayowatoa wanaume udenda,ameonekana kwenye video kadhaa za bongo fleva kama “Masogange” ya Belle 9 ambayo ilimpatiajina analolitumia mpaka leo,pia alionekana kwenye video inayofahamika kama “Msambinugwa” ya Tunda man f.t Ally Kiba.mbali na kuonekana mara kadhaa kwenye events za burudani,mrembo huyu aliingia kwenye headline za media houses Tanzania na nnje ya nchi mwaka 2013,alipokamatwa na polisi nchini Afrika Kusini akidaiwa kusafirisha kiasi kikubwa cha madawa yakulevya aina ya “Crystal

2:Zari hassan
Mrembo huyu licha ya kuwa mama wa watoto wanne,watatu wa kiume na wa kike “Princess Tiffa”aliezaa na Mogul Bongofleva star,Diamond Platnumz,ni mfanyabiashara anaemiliki magari kadhaa ya kifahari na nyumba katika nchiza Uganda na Afrika kusini,mahusiano yake na Diamond yamezidi kumfanya afatiliwe na kuzungumziwa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

1:Corazon Kwamboka
Mrembo huyu msomi aliehitimu masomoya sheria katika chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya,ni mwanamitindo aliejipatia umaarufu mara baada ya picha zake za utupu kuvuja kwenye mitandao ya kijamii,kama ilivyo kwa warembo wenzake Carazon amewahi kutokea kwenye kurasa za mbele za magazeti ya udaku nchini Kenya akihusishwa na za kutoka kimapenzi na watu maarufu na mastaa wa muziki nchini Kenya na kumfanya azidi kuandamwa na mapaparazi kila kukicha.

Teamtz.com

Dogo Mfaume naye ateketea Kwa Madawa ya Kulevya Huyu Hapa...

Wauza unga kuweni na huruma kwa watanzania wenzetu,yule Dogo Mfaume wa enzi zile za "kazi yangu ya dukani" ndo basi tena sasa hivi kashakua teja....daah vipaji vya ukweli vinazidi kupotea kwa ngada.

Mlaaniwe wote mnaouza unga kuanzia nyie wenyewe na vizazi vyenu vyote.

..."kazi yangu ya dukanii aaahahh yaniweka matataniii wanao nirudisha nyuma wengi wao majiraniii"

Saturday, 9 April 2016

Mgombea mwenza wa lowesa Juma Duni Haji Arejea CUF kisiwani zanzibar

Aliyekuwa mgombea Mwenza wa CHADEMA/UKAWA, Amerejea Cuf hii leo. Haji alikuwa mgombea Mwenza wa Edward Lowassa katika Uchaguzi wa 2015 wakipeperusha Bendera ya CHADEMA

ukweli kuhusu kifo cha Msanii wa Muziki wa dansi Ndanda Kosovo

 

Msanii wa muziki wa dansi Ndanda Kosovo amefariki dunia asubuhi ya leo katika hosptali ya taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwanamuziki mwenzake Kardinal Gento, Ndanda alikuwa alisumbuliwa na matatizo ya vidonda vya tumbo, maradhi yaliyopelekea kulazwa katika hospitali ya Mwananyamala Dar es salaam.

Kardinali ambaye pia ni mjomba wake, amesema kuwa Ndanda alihamishiwa katika Hosptali ya Taifa Muhimbili siku mbili zilizopita kutoka Mwananyamala baada ya tatizo lake kushindikana kabla ya mauti kumkuta majira ya saa mbili asubuhi ya leo.

"Nilikuwa naye hospitali tangu jana, na nimekesha naye, ilipofika asubuhi hali yake ilikuwa nafuu, nikaondoka kurudi nyumbani kwa ajili ya chakula, nikaacha anafanyiwa mpango wa damu maana alikuwa amepungukiwa damu, lakini muda mfupi baada ya kuondoka hospitali hapo nikapigiwa simu kuwa Ndanda amefariki, ilikuwa mida ya saa 2 asubuhi” Amesema Gento.

Gento amesema taratibu za mazishi zinasubiri mama yake arudi Dar es salaam, ndipo wataamua kama asafirishwe au azikwe huku
 
“Mama yake alikuwa amekwenda Lubumbashi, lakini sasa inabidi ageuze na ndege, akisharudi ndiyo tutajua kama tunazika au tunasafirisha…… mama yake ni dada yangu, kwahiyo Ndanda ananiita mimi mjomba”

Hadi mauti yanamkuta Ndada alikuwa akifanya shughuli za muziki kama msanii wa kujitegemea ‘Solo Artist’ pamoja na shughuli za kibiashara

Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein atangaza Baraza lake la Mawaziri


RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dkt. Ali Mohamed Shein leo Jumamosi, April 9, 2016 ametangaza Baraza la Mawaziri litakalosimamia kazi za serikali kwa kipindi cha uongozi wake wake kwa mujibu wa sheria.

Dkt. Shein amesema amepunguza ukubwa wa baraza hilo kutoka wizara 16 hadi kuwa wizara 13, ambapo wizara tatu amezivunja na kuzigawa ndani ya hizo wizara 13 za sasa. Mawaziri ni 13 na Manaibu waziri 7.

Ameongeza kuwa, mawaziri aliowatangaza leo atawaapisha kesho Jumapili asubuhi katika Viwanja vya Ikulu visiwani Zanzibar.

Baraza la Mawaziri Zanzibar hao ni;

1). Ofisi ya Rais na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi – Issa Haji Ussi Gavu.

2). Katiba na Sheria Utumishi wa Umma – Haroun Ali Sleiman.

3). Tawala za Mikoa na Idara maalum – Haji Omari Kheir.

4). Makamo wa 2 wa Rais – Mohamed Aboud.

5). Waziri wa Fedha na Mipango – Dk. Khalid Salum Mohamed.

6). Afya – Mahmoud Thabit Kombo.

7). Wizara ya Elimu – Riziki Pembe Juma.

8). Viwanda na Masoko – Amina Salum Ali.

9). Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi – Ali Karume.

10). Habari Utalii Utamaduni na Michezo – Rashid Ali Juma.

11). Kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi – Hamad Rashid Mohamed.

12). Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mauldine Castiko.

13). Maji Ardhi Nishati na Mazingira – Salama Aboud Talib.

CAG Aikana Ripoti Feki ya NSSF Asema Ripoti itatolewa na Bunge April 25

OFISI ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imekana taarifa inayosambazwa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya jamii kuonyesha kuna ufisadi mkubwa kwenye miradi mbalimbali ya Shirika la Taifa la Hifadhi za Jamii (NSSF).

Taarifa ya kuaminika iliyopatikana ndani ya ofisi hiyo na mmoja wa viongozi wa ofisi hiyo, wameeleza kuwa taarifa kamili kuhusiana na NSSF itatolewa na bunge April 25, mwaka huu na wanashangazwa na mambo yanayoenezwa kwenye vyombo vya habari.

Kiongozi huyo mwandamizi huku akikataa kutajwa jina lake alisema hata magazeti hayo yanayoandika uvumi huo, hakuna hata moja linaloeleza kwa ufasaha kuhusiana na ripoti ya CAG.
Ilisema watanzania wanapaswa kutulia na kusubiri taarifa rasmi itakayopelekwa bungeni, kwa kuwa imeeleza kila kitu na sio hicho ambacho kinaonekana kama kinakolezwa na watu wenye maslahi nayo.
"Hata sisi tunashangazwa kumekuwa na msukumo mkubwa na hatujui dhamira yake ni nini, ila tunachoamini tusubiri tu taarifa rasmi ya ripoti itakayopelekwa bungeni,''alisema mtoa taarifa wetu.
Akizungumza na Wabunge wajumbe wa Kamati za Bunge za usimamizi wa fedha, LAAC na PAC, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Profesa Mussa Assad kwenye semina ya mafunzo aliwaeleza wabunge kuwa Ripoti ya CAG anayo yeye na Rais Magufuli tu na anashangazwa na wanaosambaza kinachoitwa taarifa ya CAG wanapata wapi nguvu ya kufanya hivyo.

Profesa Assad alikuwa anajibu maswali ya wabunge ambapo mmoja wa Wabunge kutoka Kambi ya Upinzani alitaka maelezo ya CAG kuhusu kinachoitwa ufisadi katika NSSF.

“taratibu za ukaguzi zinajulikana. Baada ya mkaguzi kuandaa taarifa ya awali hutoa kwa mkaguliwa kujibu hoja za ukaguzi. Kisha Mkaguzi huweza kuziondoa hoja zenye majibu aliyoridhika nayo na baada ya hapo huitwa kikao kinachoitwa ‘exit meeting’ na kukubaliana masuala ya ukaguzi”, alifafanua.

Profesa Assad kwa wabunge wajumbe wa PAC,LAAC na Kamati ya Bajeti. Aliwaeleza wabunge kuwa inawezekana kinachosambazwa ni taarifa ya awali kwa malengo mahususi ambayo yeye kama CAG hawezi kuyajua na kuwataka wabunge wasubiri taarifa yake rasmi itakayowasilishwa Bungeni kabla ya tarehe 25 Aprili 2016.

Kumekuwepo na taarifa mbalimbali, ambazo nyingi zinaonekana zinamtuhumu aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau aliyeliendesha shirika hilo kwa mafanikio makubwa kuhusishwa na vitendo vya ufisadi wa miradi mbalimbali.

Baadhi ya wachunguzi wa mambo wanasema nguvu inayosukumwa kuichafua NSSF ina lengo la kufifisha nyota ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo kabla ya uzinduzi wa daraja la Kigamboni mnamo tarehe 16 Aprili 2016.

YANGA NA AL AHLY TAIFA LEO MARUDIO YA PAMBANO LA 2014, MUENDELEZO WA VITA ILIYOANZA 1982

REKODI YA YANGA NA AL AHLY

Ligi ya Mabingwa Afrika; 1982
RAUNDI YA PILI:
Al- Ahly 5-0 Yanga (Misri) 
Yanga SC 1-1 Al- Ahly (Dar) 
Ligi ya Mabingwa; 1988
RAUNDI YA KWANZA:
Yanga 0-0 Al-Ahly (Dar)
Al- Ahly 4-0 Yanga (Misri) 
Ligi ya Mabingwa; 2009
RAUNDI YA KWANZA
Al Ahly 3-0 Yanga (Misri)
Yanga 0-1 Al Ahly (Dar)
Ligi ya Mabingwa; 2014
RAUNDI YA KWANZA
Yanga SC 1-0 Al Ahly (Dar)
Al Ahly 1-0 Yanga SC (Misri)
(Yanga ilitolewa kwa penalti 4-3)
Haruna Niyonzima wa Yanga akipambana na kiungo wa Al Ahly mwaka 2014 Uwanja wa Taifa. Niyonzima hatakuwepo leo kwa sababu anatumikia adhabu ya kadi


WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga SC leo wanatupa kete yao ya kwanza katika hatua ya 16 Bora watakapomenyana na Al Ahly ya Misri Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga imerejea jana jioni Dar es Salaam kutoka kisiwani Pemba ilikokuwa imeweka kambi ya takriban wiki moja katika hoteli ya Misali Sun Set Beach, Chake Chake kujiandaa na mchezo huo.
Wapinzani wao, Ahly wapo Dar e Salaam tangu Jumatano, wakiwa wameweka kambi katika hoteli ya Serena, wakifanya mazoezi Uwanja wa Gymkhana, kabla ya jana kuhamia Uwanja wa Taifa.
Mchezo huo umekuwa ukisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini, hususan wa Yanga yenyewe kutokana na historia ya timu hizo zinapokutana. 
Hii inakuwa mara ya tano, Yanga kukutana na Ahly katika Ligi ya Mabingwa Afrika, mara zote nne za awali timu ya Jangwani, Dar es Salaam ikitolewa. 
Mara ya kwanza wababe hao walikutana mwaka 1982 katika Raundi ya Pili na Yanga ikatolewa kwa jumla ya 6-1 ikifungwa 5-0 Cairo na kulazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Mwaka 1988 zikakutana katika Raundi ya Kwanza na Yanga ikatolewa kwa jumla ya mabao 4-0 waliyofungwa Cairo baada ya kutoka sare ya 0-0 Dar es Salaam.
Mwaka 2009 Yanga wakatolewa kwa jumla ya mabao 4-0 wakifungwa 3-0 Cairo na 1-0 Dar es Salaam katika Raundi ya Kwanza pia.
Yanga ikaandika historia mwaka 2014 ilipowafunga kwa mara ya kwanza Al Ahly Dar es Salaam 1-0, bao pekee la Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kabla ya kwenda kufungwa 1-0 mjini Alexandria.
Mchezo ukarefushwa hadi dakika 120 kabla ya Ahly kushinda kwa penalti 4-3.
kwa ujumla, Yanga haijawahi kuitoa timu yoyote ya Kaskazini mwa Afrika kwenye michuano ya Afrika na Al Ahly inakuwa timu pekee ya huko kuwahi kufungwa na mabingwa hao wa Tanzania.
Mwaka 1992, Yanga ilitolewa na Ismailia ya Misri katika Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa, ikifungwa 2-0 Dar es Salaam kabla ya kwenda kulazimisha sare ya 1-1 Cairo.
Mwaka 1998 Yanga ilifungwa 6-0 na Raja Casablanca ya Morocco katika mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa kabla ya kutoa sare ya 3-3 mchezo wa marudiano Dar es Salaam.
Mwaka 2000 Yanga ililazimishwa sare ya 1-1 na Zamalek ya Misri mjini Dar es Salaam katika iliyokuwa michuano ya Kombe la Washindi kabla ya kwenda kufungwa 4-0 Cairo katika Raundi ya Kwanza.
Mwaka 2007 Yanga ilifungwa 3-0 na Esperance ya Tunisia katika hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kutoa sare 0-0 Mwanza.
Yanga iliingia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho na kutolewa na El Merreikh ya Sudan, ikitoa sare ya 0-0 Mwanza na kufungwa 2-0 Khartoum.
Mwaka 2008 Yanga ilifungwa 1-0 na Al Akhdar ya Libya mjini Tripoli kabla ya kulazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam katika Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika. 
Mwaka 2012 Yanga ililazimisha sare ya 1-1 na Zamalek ya Misri mjini Dar es Salaam, kabla ya kwenda kufungwa 1-0 mjini Cairo.
Yanga inakutana na Ahly leo ikitoka kuzitoa Cercle de Joachim ya Maurtius kwa jumla ya mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani na APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2 ikishinda 2-1 ugenini na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Al Ahly ilianzia Raundi ya Kwanza na kuitoa Recreativo do Libolo ya Angola kwa jumla ya mabao 2-1, ikitoa sare ya 0-0 ugenini kabla ya ushindi huo nyumbani.
Zote, Ahly na Yanga zimeshinda mechi nne nne na sare moja moja katika mechi tano tano zilizopita na zimeshinda mechi zote za mashindano ya nyumbani. 
Mara ya mwisho Yanga ilifungwa Januari 30, mwaka huu na Coastal Union 2-0 katika Ligi Kuu ugenini, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, wakati Ahly ilifungwa mara ya mwisho Desemba 17, mwaka jana 3-0 nyumbani na Smouha katika Ligi Kuu ya Misri.
Zote zimeshinda 2-0 dhidi ya mahasimu wao wa jadi hivi karibuni, Ahly wakiifunga Zamalek Februari 9 mabao ya Malick Evouna dakika ya 56 na Amr Gamal dakika ya 89, Yanga wakiifunga Simba Februari 20, mabao ya Donald Dombo Ngoma dakika ya 39 na Amissi Joselyn Tambwe dakika ya 72.
Zote zinafundishwa na makocha Waholanzi, Yanga ikiwa na Hans van der Pluijm mwenye umri wa miaka 67 na Ahly ikiwa na Maarten Cornelis Jol maarufu kama Martin Jol, mwenye umri wa miaka 60.
Al Ahly inaongoza Ligi ya Misri ikiwa na pointi 50 za mechi 22, wakati Yanga yenye pointi 53 za mechi 22 ni ya pili katika Ligi ya Tanzania.
Je, nani atashangilia ushindi baada ya dakika 90 leo Uwanja wa Taifa, ni Yanga au Ahly?

KASHFA YA RUSHWA TFF YATUA TAKUKURU, KAZI IMEANZA.....

 Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) tayari imeanza uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku chache baada ya kunaswa kwa sauti zinazohisiwa kuwa ni za viongozi wa TFF wakipanga matokeo ya mechi ya Ligi Daraja la Kwanza kati ya Geita Gold Sports na JKT Kanembwa.

Shirikisho hilo, tayari limemsi-mamisha kazi msaidizi wa Rais, Juma Matandika huku Kaimu Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Martin Chacha akitangaza kujiuzulu nafasi yake.

Ofisa Habari wa Takukuru, Tunu Mlei alisema kisheria suala hilo kwa hivi sasa hawaruhusiwi kulizungumza na wataliweka wazi mara baada ya uchunguzi kukamilika.

 “Takukuru tayari imeanza uchunguzi wa hizo tuhuma za rushwa inayodhaniwa TFF inahusika, hivyo hilo suala lipo kwetu na linashughulikiwa kisheria haturuhusiwi kulizungumza hadi pale litakapokamilika, hivyo tunawaomba wadau wa soka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki tukisubiria uchunguzi huo utakapomalizika,” alisema Mlei.