Rais Dr Jakaya Kikwete akimfariji mtoto wa Dr Wiliam Mgimwa Bw Godfrey
Mgimwa wakati wa mazishi ya babake hivi karibuni ,mtoto huyo ndie
mshindi wa kura za maoni ubunge jimbo la kalenga kupitia CCM.
...................................................................................
IKIWA ni siku tatu zimepita toka wana CCM jimbo la Kalenga kumchagua
kwa kura za kishindo Godfrey Mgimwa ambae ni mtoto wa aliyekuwa
mbunge wa jimbo la Kalenga marehemu Dr Wiliam Mgimwa hali ya kisiasa
ndani ya CCM Kalenga si shwari baada ya ushindi wa mtoto huyo wa Dr
Mgimwa kuonyesha kuwagawa wananchi na wana CCM.
Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu wa katika maeneo mbali mbali ya jimbo hilo baada ya
ushindi huo mkubwa alioupata mtoto wa Dr Mgimwa wengi wanaonyesha
kuwapinga wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM ambao waliamua kumpigia
kura Mgimwa kwa madai kwa kufanya hivyo ni sawa na kulitoa sadaka
jimbo hilo kwa vyama vya upinzani.
Ajuaye Kalinga alisema kuwa upinzani
katika jimbo la Kalenga haupo kabisa ila kutokana na uamuzi mbaya
uliofanywa na wajumbe hao wa CCM kwa kumchangua mrithi wa Dr Mgimwa
kuwa ni mtoto wake ni wazi upinzani utaingizwa Kalenga na wana CCM
wenyewe ambao hawaungi mkono uamuzi huo.
Kalinga alisema ni heri angechaguliwa
mwana CCM mwingine kata ya wanachama tisa waliojitokeza kuliko
kumchagua mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwani kwa kufanya
hivyo ni wazi CCM itapoteza sifa na kuingia katika wakati mgumu kwa
kuendekeza siasa za kubebana na siasa za kifamilia.
" Tunashindwa kujua wajumbe wa mkutano
huo wa kura za maoni jimbo la Kalenga walikutwa na nini hadi kuamua
kutoa kura za rambi rambi kwa mtoto wa mbunge Dr Mgimwa ....siku zote
CCM tumekuwa tukiutumia udhaifu wa Chadema wa kukifanya chama hicho
kuwa cha watu wa Kaskazin kwa maana ya wachaga wakati leo CCM
tunauonyesha umma kuwa CCM Kalenga ni mali ya familia ya akina Dr
Mgimwa "alisema
Kuwa mbali ya kuwa kumkata jina la
mtoto wa Dr Mgimwa itapelekea waliomchagua kuchukia uamuzi huo ila
ni heri kufanya hivyo kwa kukifanya chama hicho kuondokana na aibu ya
kuwa chama cha ukoo kuliko kumkumbatia kwa kumfuta machozi mtoto wa
Dr Mgimwa jambo ambalo ni hatari ni njia kwa upinzani kutumia nafasi
hiyo kuuthibitishia umma kuwa CCM ni chama cha familia na viongozi na
watoto wao.
Hata hivyo alisema kuwa wananchi wa
kalenga ambao ni wana CCM wasio viongozi wala wajumbe wamepanga
kukutana mara baada ya uteuzi wa mwisho wa CCM ili kutoa msimamo wao
juu ya suala hilo kama CCM iendelee kuongoza jimbo hilo ama
kuelekeza kura zao kwa Chadema .
"Sisi kama wana kalenga kweli
hatujapendezwa na uamuzi wa wenzetu waliokwenda mjini kushiriki
kuchagua ....sasa wale walikuwa na nafasi ndani ya chama ila sisi
tusio na nafasi ya kushiriki kuchagua ndani ya CCM tutatoa uamuzi wetu
mgumu na tunaomba wajumbe wote zaidi ya 800 walioshiriki kura za
maoni kura zao wampe mtoto wa Mgimwa ila sisi wananchi zaidi ya
200,000 jimbo la kalenga tunajua kwa kupeleka kura zetu...kwani kura
ni siri yetu"
Huku Yohana Sanga akidai kuwa kilichotokea jimbo la Arumeru Mashariki kwa kumpeleka bungeni mgombea wa Chadema Joshua
Nassar ndicho kitakachotokea katika jimbo la Kalenga kwa kuipumzisha
CCM kwa kipindi hiki kifupi cha mwaka mmoja na nusu hadi 2015 kwa
kumchangua mgombea wa Chadema hata akiwa ni mpiga debe stendi watampa
kura zao kuliko kubariki siasa za kifamilia katika jimbo hilo.
"
Tunakipenda sana chama chetu CCM na ndio sababu ya jimbo la Kalenga
hata upinzani hauna nguvu ukilinganisha na maeneo mengine ila katika
hili lazima wana Kalenga tuseme basi yatosha kwa wajumbe wa Halmashauri
kuu ya CCM jimbo kutuchagulia mgombea ambae ni mtoto wa marehemu
sisi tuna uamuzi wetu ila sio kauli ya kupenda bonga penda na ua
lake....tulipenda bonga Dr Mgimwa ila Mungu kampenda zaidi yetu na sio
kulazimisha upendo kwa ua lisilo zaa matunda kwetu kwani kuendelea
kumpa kura za rambi rambi mtoto wa Dr Mgimwa ni sawa na kukaa katika
tawi la mti unalolikata mwenyewe "
Alisema
wana Kalenga wapo tayari kumpigia kura mgombea yeyote wa CCM kati
ya wagombea 9 walioingia katika mnyukano huo ila si mtoto wa Dr
Mgimwa kwani ubunge si nafasi za kurithiana kifamilia na si kweli
kuwa ukoo wa Dr Mgimwa ndio wenye nafasi ya kuendelea kuongoza jimbo
hilo .
"
Tunajua kauli mbali mbali za viongozi wakati wa mazishi ikiwemo ile
ya katibu mkuu wa CCM na waziri mkuu kuwa wataendelea kuisaidia
familia ya Dr Mgimwa ila kama msaada wenyewe ndio wa kupeana nafasi za
uongozi wana Kalenga tunasema msaada huo ni kaa la moto kwa CCM ni
wasije tafuta mchawi baada ya matokeo "
Katika
uchaguzi huo wa kura za maoni Mtoto wa Mgimwa alishinda kwa kura 342
huku Jackson Kiswaga akipata kura 170 na mkuu wa wilya ya Pangani Hafsa
Mtasiwa akiambulia kura 42 .
Wagombea
wengine ni pamoja na Peter Mtisi akipata kura 33 ,Msafiri Pangagira
kura 8,Bryson Kibasa kura 7,Edward Mtakimwa kura 3 na Thomas Mwiluka
akiambulia kura 2.













0 comments:
Post a Comment