Japokuwa hakutaja moja kwa moja kuhusu tuhuma zinazoikabili Serikali yake kuhusiana na mauaji ya aliyewahi kuwa Mkuu wake wa Ujasusi aliyeuawa Januari mosi akiwa hotelini huko Afrika Kusini, Patrick Karegeya, alisema wale wote wanaoigeuka nchi yao na kuchagua kuua raia wasio na hatia kwa sababu zao binafsi wanastahili kushughulikiwa ipasavyo.
"Sitakuwa na huruma na watu ambao wanasahau namna Rwanda ilivyowatengeneza na kuwa hapo walipo na hatimaye wanaamua kuisaliti kwa kuua raia wa Rwanda wasio na hatia, wakiwemo kinamama na watoto," aliongeza.
Alisema Rwanda haina sababu ya kuhusishwa au kuwajibishwa kwa ajili ya wale walioamua kuchukua njia zaidi na kufanya mambo yao kwa nia ya kuharibu yale yaliyofanyika kwa ajili ya kuliimarisha taifa la Rwanda.













0 comments:
Post a Comment