MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Saturday, 1 February 2014

KALLSTROM: MPYA ARSENAL MAJERUHI KABLA KUANZA KUCHEZA!

KIM_KALLSTROMMCHEZAJI MPYA wa Arsenal, Kim Kallstrom, atakuwa nje kwa muda baada kugundulika ameumia Mgongo.
Kallstrom, Miaka 31, inadaiwa aliumia Mazoezini Jumanne huko Abu Dhabi, UAE, wakati alipokuwa na Klabu yake Spartak Moscow na aliwaeleza Arsenal matatizo yake hapo Jana alipotua London kwa upimwaji Afya lakini Vipimo vya MRI havikuonyesha tatizo lakini Kipimo cha CT kilionyesha lipo tatizo kwenye Mgongo wake.
Inadaiwa Wenger alijulishwa taarifa hizi lakini ikaamuliwa wakamilishe Usajili wake hiyo Jana ambayo ndio ilikuwa Siku ya mwisho ya Uhamisho wa Wachezaji kwenye Dirisha la Uhamisho la Januari.
Inakisiwa Kallstrom atazikosa Mechi 6 za Arsenal ambazo ni dhidi ya Crystal Palace, Liverpool, mara mbili, Manchester United, Bayern Munich na Sunderland.
Kallstrom, Raia wa Sweden aliewahi kuichezea Lyon ya France, ndie Mchezaji pekee
aliesainiwa na Arsenal kwenye Dirisha la Uhamisho la Januari na amesainiwa kwa Mkopo hadi mwishoni mwa Msimu ili kuziba pengo la Viungo Majeruhi Aaron Ramsey na Jack Wilshere pamoja na Mathieu Flamini ambae amefungiwa Mechi 3 baada Kadi Nyekundu.
Mchezaji huyo sasa anatarajiwa kurudi kwao Sweden kisha kwenda Urusi na baadae kurudi London kuendelea na Matibabu akiwa na Arsenal.

LA LIGA: BARCA YAPIGWA NA VALENCIA BAO 3-2 KWAO NOU CAMP

>>JUMAPILI: ATLETICO AU REAL KUTWAA UONGOZI?!

LA LIGA sasa ni mshikemshike kweli baada ya Leo Valencia kufanya kweli Uwanjani Nou Camp na kuichapa Barcelona Bao 3-2 na kuwaweka Mabingwa hao kwenye njia panda maana Jumapili Atletico Madrid au Real Madrid zina nafasi kubwa kuwapiku uongozi wa Ligi.

MSIMAMO-Timu za Juu:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 FC Barcelona 22 17 3 2 59 16 43 54
2 Atletico de Madrid 21 17 3 1 52 14 38 54
3 Real Madrid CF 21 17 2 2 60 21 39 53
4 Athletic de Bilbao 21 13 3 5 41 27 14 42

MESSI_v_RonaldoBarca walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 7 Mfungaji akiwa Alexis Sanchez na Valencia kujibu na kupiga Bao mbili katika Dakika ya 44 lililofungwa na Parejo na Dakika 4 baadae kupitia Pablo Piatti.
Barca walisawazisha kwa Penati ya Lionel Messi na hilo ni Bao lake la kwanza baada kutofunga katika Mechi 3 lakini Paco Alcácer, katika Dakika ya 59, aliipigia Valencia Bao la 3 na kuwapa ushindi.
Barca walimaliza wakiwa Mtu 10 baada Jordi Alba kupewa Kadi ya Njano ya pili kwenye Dakika ya 78 na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Ukiiondoa Real Madrid, Valencia imekuwa Timu ya kwanza kuondoka Nou Camp bila kufungwa tangu Oktoba 2011 Sevilla ilipopata Sare ya 0-0.
Matokeo haya yameiacha Barca uongozini ikiwa Pointi 54, sawa na Atletico Madrid, lakini Atletico wana Mechi moja mkononi ambayo watacheza Nyumbani kesho Jumapili na Real Sociedad wakati Real Madrid, walio Pointi 1 nyuma ya Barca na Atletico, pia watacheza Jumapili Ugenini na Athletic Bilbao.
Atletico na Real zina nafasi nzuri kuitungua Barca toka kileleni.

RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Ijumaa Januari 31
Granada CF 1 Celta de Vigo 2
Jumamosi Februari 1
FC Barcelona 2 Valencia 3
Levante v Rayo Vallecano
Getafe CF v Real Valladolid
Malaga CF v Sevilla FC
Jumapili Februari 2
Elche CF v UD Almeria
Real Betis v RCD Espanyol
Atletico de Madrid v Real Sociedad
Athletic de Bilbao v Real Madrid CF
Jumatatu Februari 3
Villarreal CF v Osasuna

UVCCM MKOA WA MBEYA WAMTAKA JOHN SAMWEL MALECELA ASINGILIE MASWALA YA VIJANA NDANI YA CCM

WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwa katikati ya sherehe za maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa kwake, baadhi ya vijana ambao ni wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM) mkoa wa Mbeya wameibuka wakiwa na mabango kumshinikiza Waziri Mkuu mstaafu John Samwel Malecela kuacha kuingilia masuala ya vijana ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

Mwenyekiti wa mkutano huo Msumba Mdesa wa Mbeya mjini


 Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa kupitia UVCCM mkoa wa Mbeya, Rabson Mwaipula alisema kuwa Malecela ni kiongozi aliyestaafu hapaswi kuingilia masuala ya vijana na badala yake akae atulie na kula pensheni yake kwa amani.



Edward Kakwale toka Momba


David Mwakalinga, ambaye alijitambulisha kuwa ni Mwenyekiti wa UVCCM kata ya Maendel.eo Jijini Mbeya, alisema Makonda anapaswa kujua hisitoria za viongozi wa wa juu wa CCM badaya ya kuibuka kwenye vyombo vya habari na kuropoka.

















WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwa katikati ya sherehe za maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa kwake, baadhi ya vijana ambao ni wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM) mkoa wa Mbeya wameibuka  wakiwa na mabango kumshinikiza Waziri Mkuu mstaafu John Samwel Malecela kuacha kuingilia masuala ya vijana ndani ya Chama Cha Mapinduzi.


Vijana hao pia wamemtaka Katibu wa Uenezi wa UVCCM, Paulo Makonda kumwomba radhi Lowassa kwa maneno aliyoyatoa hivi karibuni kwenye vyombo vya habari kwa madai hawakumtuma afanye hivyo na kauli zake zinalenga kukigawa chama.

 Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa kupitia UVCCM mkoa wa Mbeya, Rabson Mwaipula alisema kuwa Malecela ni kiongozi aliyestaafu hapaswi kuingilia masuala ya vijana na badala yake akae atulie na kula pensheni yake kwa amani.

“Malecela kwa hili amekuwa kama mchezaji ambaye yupo uwanjani lakini hajui anacheza namba ngapi na hajui anacheza na nani, tunamshauri aache kucheza mchezo ambao haumfai na badala yake atulie atushauri vizuri, sisi vijana yale tunayo tenda” alisema Mwaipula.

Alisema kitendo cha Malecela kuanza kuingilia kati masuala ya vijana na kumshambulia Waziri Mkuu mwenzake mstaafu, Edward Lowassa kinaonyesha jinsi Malecela asivyotumia vizuri busara zake kukiunganisha chama na badala yake anakigawa.

Alisema Malecela kama anataka aache posho anazolipwa kama Waziri Mkuu Mstaafu arejee kwenye ulingo wa Siasa kwani anaonekana bado anautamani licha ya kuangushwa vibaya kwenye jimbo lake la Mtera mwaka 2010.

Mwanachama mwingine wa UVCCM, Kisumba Mdesa ambaye alikuwa mwenyekiti wa mkutano wa vijana hao na wandishi wa habari jana jijini Mbeya alisema Makonda haijui vizuri CCM na historia ya viongozi wa CCM katika mchango wao wa kukijenga chama, hivyo kitendo chake cha kumshambulia Lowassa kwenye vyombo vya Habari ni utovu wa nidhamu.

Alisema kuwa Makonda hana sifa ya kuizungumzia UVCCM kwa kuwa yeye alichaguliwa kuongoza Chipukizi, lakini yeye amejingiza na kujifanya kuwa ni msemaji wa UVCCM.

Naye David Mwakalinga, ambaye alijitambulisha kuwa ni Mwenyekiti wa UVCCM kata ya Maendel.eo Jijini Mbeya, alisema Makonda anapaswa kujua hisitoria za viongozi wa wa juu wa CCM badaya ya kuibuka kwenye vyombo vya habari na kuropoka.

Alisema kiongozi kama Lowassa, amefanya mambo makubwa hapa nchini hasa kwa kusimamia maamuzi magumu, pamoja na miradi ya maendeleo kama shule za kata.

Alisema enzi za uongozi wa Lowassa kama waziri Mkuu alisimamia kwa nguvu zote ujenzi wa shule za kata ambazo sasa zimeonesha matunda kwa vijana wa kitanzania kupata elimu katika mazingira safi na kwa gharama nafuu.

Kutokana na hali hiyo wote kwa pamoja waliwaomba radhi viongozi wa dini, kwani maneno yaliyotewa na wenzao hao ndani ya chama hicho si msimamo wa wanachama wote.

Kwa hisani ya Mbeya yetublog
 

YUSUF MANJI AWAWAKIA WANOOMUANDAMA SEIF MAGARI

 
index 
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji amewaonya wanachama na mashabiki wa timu hiyo wanaotishia maisha Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano ya imataifa wa klabu hiyo, Seif “Magari” Ahmed kuwa sheria kali zitachukuliwa dhidi yao.
Katika taarifa yake aliyoitoa jana, Manji amesema kuwa si suala jema kwa wanachama kumuhusisha Seif na matokeo ya timu hiyo ambayo kwa sasa imeshinda mechi moja na kutoka sare mechi moja katika mzunguko wa pili wa Ligi kuu ya Tanzania Bara.
Manji amesema kuwa madai kuwa Seif siyo mwanachama halali  wa Yanga hayana msingi wowote na kuyaita madai hayo kuwa ni ya uzushi na yanaenezwa na maadui zao ambao hawaitakii Yanga mema.
 
Alisema kuwa hivi karibuni kumekuwa na madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu, taarifa za hujuma ndani ya timu ambazo zimewahusisha uongozi na baadhi ya wanachama jambo ambalo si la kweli.
Alifafanua kuwa ni haki kwa kwa nia njema kwa wanachama kuhoji mwenendo wa timu yao pale wanapoona-hairidhishi na ni wajibu wa wanachama kuchanganua mawazo merna na mabaya na siyo kumuhisha mtu kwa moja kwa moja kutokana na mtazamo hasi walionao.
“Ushindi au mwenendo mzuri  wa timu unatokana na viwango vizuri, nidhamu na ushirikiano wa wahusika wote, wachezaji, walimu, viongozi, wanachama na wapenzi kwa ujumla. Uongozi ulikutana na wachezaji, walimu, baadhi ya wanachama na wapenzi na kuyazungumzia na kukubaliana kuhusu mapungufu yaliyojitokeza kwa wahusika wote na kuchukua hatua ya kubadilisha benchi la ufundi,” alisema Manji.
Aliongeza kwa kusema kuwa uongozi ulifika mbali zaid kwa kutoa adhabu na onyo kali kwa baadhi ya wachezaji walionyesha utovu wa nidhamu kwa kipindi kilichopita na kusikitishwa kuona kuwa baadhi ya wadau kwa kutumia vyombo vya habari wanachochea na kutengeneza uhasama ambao kwa kweli haupo ama kwa faida zao binafsi, au kwa kutumiwa na watu ambao hawana nia njema kwa klabu.
Manji pia aliwaomba wadau wote wanamichezo na hasa wahariri wa michezo kudhibiti matumizi mabaya ya watu au vyombo vya habari yanayochangia sana kuzorotesha michezo nchini.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA JUMUIYA YA ISTIQAAMA DAR.

  

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed  Gharib Bilal, akuhutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Jumuiya ya Istiqaama, uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, leo Feb 01, 2014. Picha na OMR 004 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kufungua rasmi Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Istiqaama, leo Feb 01, 2014. Picha na OMR
Baadhi ya Wanachama wa Jumuiya ya Istiqaama, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akihutubia kufungua rasmi Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo leo katika Ukumbi wa Karimjee. Picha na OMR 006 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, baada ya kufungua rasmi Mkuu wa Jumuiya hiyo leo katika Ukumbi wa Karimjee. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, baada ya kufungua rasmi Mkuu wa Jumuiya hiyo leo katika Ukumbi wa Karimjee. Picha na OMR
8 
Picha ya pamoja baada ya kufunguliwa mkutano huo.

MWENYEKITI WA CCM DR. JAKAYA KIKWETE AWASILI SALAMA MBEYA KWA MAADHIMISHO YA MIAKA 37 YA CCM

1Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akishuka kwenye ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya mara baada ya kuwasili rasmi mkoani humo tayari kwa kuongoza maadhimisho ya Miaka 37 ya Chama cha Mapinduzi yanayofanyika kesho kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, ambapo amepokelewa na viongozi mbalimbali wa kitaifa wa Chama na Serikali pamoja na wananchi waliojitokeza katika mapokezi hayo.   2Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Godfrey Zambi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Songwe. 3Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Abas Kandoro na Mkuu wa wilaya ya Mbeya mjini Dr. Norman Sigalla kushoto. 4Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Marck Mwandosya Waziri asiyekuwa na Wizara maalum, katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dr. Norman Sigalla na kushoto ni Dr. Harrison Mwakyembe Waziri wa Uchukuzi. 5Mwenyekiti wa Cma Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Kamnda wa Polisi mkoa wa Mbeya SACP AHMED Z. MSANGI . 7Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr.Jakaya Kikwete akipokea heshima kutoka kwa kikosi cha vijana wa Chipukizi mkoa wa Mbeya mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Songwe kulia ni  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Godfrey Zambi na kutoka kushoto ni  Dr. Harrison Mwakyembe Waziri wa Uchukuzi, Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Abas Kandoro, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya mjini Dr. Norman Sigalla na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana 8Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr.Jakaya Kikwete akivishwa skafu na vijana wa chipukizi mkoa wa Mbeya mara baada ya kuwasili mkoani humo kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 10Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa serikali na chama. 11Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na  viongozi na wabunge 12Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na vijana wa UVCCM. 13 14Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dr. Jakaya Kikwete akiwa katika kikao cha ndani na viongozi wa CCM mkoa wa Mbeya kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Mzee Philip Mangula Makamu Mwenyekiti Bara na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Godfrey Zambi 15wajumbe wa harmashauri kuu mkoa wa Mbeya wakiwa katika kikao hicho.16 
Mary Mwanjelwa Mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Mbeya akisalimiana na makada wa chama hicho kushoto ni Kada wa CCM Richard Kasesela. 17 
Ndege ya Rais Jakaya Kikwete ikiwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya

HII NI RASIMI WAYNE ROONEY SASA KUBAKI MAN UNITED

rooney1 337d8

 

MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney amekubali kusaini mkataba mpya utakaomweka Old Trafford zaidi ya mwaka 2015 huku akiwa mchezaji anayelipwa zaidi klabuni hapo. 
Rooney amesuasua kusaini mkataba mpya Old Trafford na ilidaiwa kwamba alikuwa anajiandaa kuondoka mwishoni mwa msimu kwa ajili ya kupata changamoto mpya ya soka nje ya Man United.
Mkataba wa Rooney unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao Juni 2015 na kulikuwa na wasiwasi kwamba staa huyo wa zamani wa Everton alikuwa anataka kuondoka bure mwishoni mwa msimu ujao hili apate fedha nyingi zaidi.
Hata hivyo, kocha David Moyes amefanikiwa kumshawishi nyota huyo kubaki lakini kwa gharama za kumlipa mshahara wa Pauni 300,000 (Sh.750 milioni) kwa wiki ambao unaweza kuwa wa mwisho kwake klabuni hapo.
Wakati huohuo, licha kumnasa kiungo mchezeshaji wa Chelsea, Juan Mata na kufanikiwa kumbakiza Rooney, Moyes amekumbana na pigo baada ya kiungo wa Juventus aliyekuwa anamwinda, Arturo Vidal kusisitiza kwamba atabaki klabuni hapo.
Moyes ameshasafiri mpaka Italia kwa ajili ya kumwangalia nyota huyo wa kimataifa wa Chile ambaye yupo katika kiwango cha juu na alikuwa anataka kumchukua katika kikosi chake kwa ajili ya kukitia makali na kukirudisha katika ushindani.
Moyes atalazimika kuongeza juhudi zake kwa kiungo wa Bayern Munich, Toni Kroos ambaye anaweza kuuzwa. Chanzo: mwanaspoti